Nusu fainali Kombe la shirikisho, Chama atakuwa Arusha, Diarra Mwanza  

Na Winfrida Mtoi

MCHEZO wa nusu fainali ya kwanza ya Kombe la Shirikisho kati ya Simba na Coastal Union unatarajiwa kuchezwa Juni 20, 2026 katika Uwanja wa Sheikh Amri Abeid, jijini Arusha, wakati Yanga itakutana na Azam FC  nusu fainali ya pili, dimba la CCM Kirumba, jijini Mwanza, Juni 21, 2026.

Taarifa hiyo imetolewa leo Jumatatu, Mei 18, 2026 na Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), ikiwa ni siku moja baada ya kumalizika kwa michezo ya robo fainali.

Simba imetinga nusu fainali baada ya jana Mei 17, 2026 kuichapa TRA united mabao 4-0 katika  mchezo uliopigwa KMC Complex, jijini Dar es Salaam. Yanga iliifunga JKT Tanzania mabao 2-0 Uwanja wa Maj. Gen. Isamuhyo.

Azam FC iliichapa Mashujaa bao 1-0  jana katika Uwanja wa Lake Tanganyika, Kigoma, huku Coastal Union ikitinga nusu fainali kwa kuiondosha  Singida Bs kwa ushindi wa mikwaju ya penalti 4-2 baada ya kutoka suluhu ndani ya dakika 90, kwenye dimba la Mkwakwani Tanga.

spot_img

Latest articles

Rais Samia aunda Tume ya Uchunguzi wa Kijinai ghasia za Oktoba 29

Na Mwandishi Wetu RAIS Samia Suluhu Hassan, ameunda Tume ya Uchunguzi wa Kijinai wa matukio...

Tanesco yatakiwa kubuni teknolojia mpya kuboresha huduma kwa wateja

Na Mwandishi Wetu NAIBU Waziri wa Nishati, Salome Makamba, ameielekeza TANESCO kuendelea kufanya tafiti...

DAWASA yaja na operesheni siku 90 kudhibiti upotevu wa maji

Na Mwandishi Wetu MAMLAKA ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es Salaam (DAWASA)...

DAS Temeke azindua ofisi ya Wilaya ya kitanesco ya Mikwambe

📌Aipongeza TANESCO kwa maboresho yanayoendelea ili kusogeza huduma karibu kwa Wananchi. 📌Asema itapunguza adha wananchi...

More like this

Rais Samia aunda Tume ya Uchunguzi wa Kijinai ghasia za Oktoba 29

Na Mwandishi Wetu RAIS Samia Suluhu Hassan, ameunda Tume ya Uchunguzi wa Kijinai wa matukio...

Tanesco yatakiwa kubuni teknolojia mpya kuboresha huduma kwa wateja

Na Mwandishi Wetu NAIBU Waziri wa Nishati, Salome Makamba, ameielekeza TANESCO kuendelea kufanya tafiti...

DAWASA yaja na operesheni siku 90 kudhibiti upotevu wa maji

Na Mwandishi Wetu MAMLAKA ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es Salaam (DAWASA)...