Didier Drogba atikisa Bunge la Tanzania

Na Mwandishi Wetu

Shangwe​  zimetawala  katika Ukumbi wa Bunge jijini Dodoma leo Mei 4, 2026,   baada ya gwiji wa soka duniani na nahodha wa zamani wa timu ya Taifa ya Ivory Coast na mchezaji wa Chelsea,  Didier Drogba kutambulishwa mbele ya  wabunge na wageni waalikwa.

​Drogba, ambaye aliwasili nchini jana kwa mwaliko rasmi wa Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo,  Paul Makonda, amepata mapokezi ya kipekee na kuwa kivutio bungeni.

​Lengo la ziara ya nyota huyo mwenye umri wa miaka 48, ambaye miongoni mwa wachezaji bora walioweka alama katika soka  barani Afrika na duniani,  ni kuunga mkono jitihada za kukuza michezo na utalii nchini.

Drogba anakumbukwa kama mshambuliaji mwenye nguvu na ushawishi mkubwa, hasa katika klabu ya Chelsea ambako alicheza kwa mafanikio makubwa.

​Klabu nyingine alizowahi kuchezea nyota huyo ni ​​Olympique Marseille (Ufaransa), ​Shanghai Shenhua (China), ​Galatasaray (Uturuki), ​Montreal Impact (Canada/MLS) na ​Phoenix Rising (Marekani)

spot_img

Latest articles

Sangweni: Sekta ya Mafuta na Gesi Ni Chachu ya Ukuaji wa Uchumi wa Taifa

Na Mwandishi Wetu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Udhibiti Mkondo wa Juu wa Petroli...

VETA Kihonda yaja ‘cold room’ kupunguza upotevu wa mazao ya wakulima

Na Mwandishi Wetu UBUNIFU wa mfumo jumuishi wa kuhifadhi mazao kwa kutumia teknolojia ya ubaridi...

Ofisi ya Msajili wa Hazina yalenga kukusanya Sh2 trilioni mwaka 2026/27

Na Mwandishi Wetu OFISI ya Msajili wa Hazina (OTR) imejiwekea lengo la kukusanya Sh2...

MAULIDI KITENGE AUNGANA NA TANESCO KUHAMASISHA NISHATI SAFI YA KUPIKIA KWA UMEME

📌 Aahidi kutumia jukwaa lake kuhamasisha wananchi kutumia umeme kwa shughuli za kupikia 📌 Ushirikiano...

More like this

Sangweni: Sekta ya Mafuta na Gesi Ni Chachu ya Ukuaji wa Uchumi wa Taifa

Na Mwandishi Wetu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Udhibiti Mkondo wa Juu wa Petroli...

VETA Kihonda yaja ‘cold room’ kupunguza upotevu wa mazao ya wakulima

Na Mwandishi Wetu UBUNIFU wa mfumo jumuishi wa kuhifadhi mazao kwa kutumia teknolojia ya ubaridi...

Ofisi ya Msajili wa Hazina yalenga kukusanya Sh2 trilioni mwaka 2026/27

Na Mwandishi Wetu OFISI ya Msajili wa Hazina (OTR) imejiwekea lengo la kukusanya Sh2...