Na Mwandishi Wetu
Shangwe zimetawala katika Ukumbi wa Bunge jijini Dodoma leo Mei 4, 2026, baada ya gwiji wa soka duniani na nahodha wa zamani wa timu ya Taifa ya Ivory Coast na mchezaji wa Chelsea, Didier Drogba kutambulishwa mbele ya wabunge na wageni waalikwa.
Drogba, ambaye aliwasili nchini jana kwa mwaliko rasmi wa Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Paul Makonda, amepata mapokezi ya kipekee na kuwa kivutio bungeni.
Lengo la ziara ya nyota huyo mwenye umri wa miaka 48, ambaye miongoni mwa wachezaji bora walioweka alama katika soka barani Afrika na duniani, ni kuunga mkono jitihada za kukuza michezo na utalii nchini.
Drogba anakumbukwa kama mshambuliaji mwenye nguvu na ushawishi mkubwa, hasa katika klabu ya Chelsea ambako alicheza kwa mafanikio makubwa.
Klabu nyingine alizowahi kuchezea nyota huyo ni Olympique Marseille (Ufaransa), Shanghai Shenhua (China), Galatasaray (Uturuki), Montreal Impact (Canada/MLS) na Phoenix Rising (Marekani)


