TAFF yajipanga kwa Ligi Kuu, Tabora yaanzisha timu

Na Mwandishi Wetu

MKURUGENZI wa ufundi Shirikisho la Mpira wa Miguu kwa Watu wenye Ulemavu (TAFF), Shaban Msangi ameitembelea timu mpya ya soka kwa watu wenye ulemavu ya Unyanyembe mkoani Tabora ikiwa ni maandalizi ya Ligi Kuu Soka, itakayoanza Julai, 2026, jijini Dar es Salaam.

Msangi amesema kutembelea timu hiyo ni moja ya juhudi za shirikisho katika kukuza mchezo wa soka kwa watu wenye ulemavu kwa kuhakikisha wanaifikia mikoa mingi  ili kupata idadi kubwa ya timu kuelekea katika ligi hiyo.

Hata hivyo amesema kuna changamoto wanayokutana nayo, kwa mfano katika timu hiyo ya Unyanyembe kuna uhaba wa vifaa vya michezo kama vile jezi, viatu na magongo na kuwaomba wadau kujitokeza kutoa sapoti.

“Kama tunavyojua mchezo huu ni kwa watu wenye ulemavu, ni watu wenye mahitaji  maalum, ni mchezo ambao umebeba zaidi hisia za watu,” ameeleza Msangi.

Kwa upande wake kocha wa timu hiyo ya Unyanyembe, Hamad Simba amesema wanaendelea na mazoezi ya kujiandaa na ligi hiyo, huku akiwahimiza wakazi wa mkoa huo kupeleka vijana kujiunga na timu.

“Tuna nafasi bado vijana waliopo wilayani, popote pale mkoa wa Tabora waje wajiunge na timu nafasi bado ipo. Lakini pia ombi langu nikipata msaada wa vifaa itasaidia zaidi kujenga timu hii,” amesema.

spot_img

Latest articles

Rais Samia: Serikali itachukua hatua yaliyopendekezwa na CAG

Na Mwandishi Wetu RAIS Samia Suluhu Hassan amesema Serikali itachukua hatua kama ilivyoelekezwa na sheria...

Bwege afariki dunia

Na Mwandishi Wetu MBUNGE wa zamani wa Jimbo la Kilwa Kusini, Mkoani Lindi, Selemani Bungara...

Ripoti ya CAG yaibua mazito ujenzi wa uwanja wa AFCON Arusha

Na Mwandishi Wetu RIPOTI ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), Charles...

Deni la Serikali lafikia trilioni 110, mikopo yatajwa

Na Mwandishi Wetu MDHIBITI na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), Charles Kichere, amesema...

More like this

Rais Samia: Serikali itachukua hatua yaliyopendekezwa na CAG

Na Mwandishi Wetu RAIS Samia Suluhu Hassan amesema Serikali itachukua hatua kama ilivyoelekezwa na sheria...

Bwege afariki dunia

Na Mwandishi Wetu MBUNGE wa zamani wa Jimbo la Kilwa Kusini, Mkoani Lindi, Selemani Bungara...

Ripoti ya CAG yaibua mazito ujenzi wa uwanja wa AFCON Arusha

Na Mwandishi Wetu RIPOTI ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), Charles...