Senegal yavuliwa ubingwa wa AFCON 2025, wapewa Morocco

Na Mwandishi Wetu

SENEGAL imevuliwa ubingwa  wa Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON) 2025 baada ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Afrika (CAF) kubatilisha matokeo na kuwapa ubingwa huo Morocco.

Uamuzi huo ni kutokana na rufaa iliyowasilishwa na Shirikisho la Soka la Morocco (FRMF), ambapo CAF imesema imekubalika kisheria na imeamuliwa kwa faida yao.

CAF imewapa ushindi Morocco katika rufaa hiyo na ‘ushindi wa mezani’ wa mabao 3-0, hivyo Senegal kutakiwa kurejesha kombe na medali, ili wakabidhiwe mabingwa wapya, ambao sasa ni Morocco.

Maamuzi hayo yanaelezwa kuwa ni kutokana na Senegal kugomea mchezo kwa dakika kadhaa kutokana na Morocco kupewa penati iliyopigwa na Ibrahim Diaz.

Katika taarifa ya CAF imesema kuwa Senegal ilikiuka Kifungu cha 82 cha kanuni za AFCON, jambo lililosababisha kutumika kwa Kifungu cha 84.

Kifungu cha 82 kinaeleza kuwa ikiwa timu itakataa kucheza au itaondoka uwanjani kabla ya muda wa kawaida kuisha bila ruhusa ya mwamuzi, itachukuliwa kama imepoteza na itaondolewa kwenye mashindano.

Kifungu cha 84 kinaongeza kuwa timu yoyote itakayokiuka Kifungu cha 82 itaondolewa kabisa kwenye mashindano na kupoteza mechi hiyo kwa mabao 3-0.

spot_img

Latest articles

Yanga kuikabili TRA bila Depu, kocha aeleza ugumu ulipo

Na Mwandishi Wetu WAKATI Yanga ikitarajiwa kushuka dimbani kesho Machi 18, 2026  kuikabili TRA United katika Ligi...

Vijana 3,967 waomba uwezeshaji kupitia Go Green na IMBEJU ya CRDB Bank Foundation

Na Mwandishi wetu JUMLA ya vijana 3,967 kutoka maeneo mbalimbali nchini wamewasilisha maombi ya...

RC Kunenge aipongeza Dawasa, awapa jukumu madiwani

Na Mwandishi wetu MKUU wa Mkoa wa Pwani, Abubakar Kunenge amesema ushirikishwaji wananchi kwenye...

Serikali yatoa maelekezo nane kuimarisha kampuni ambazo ina umiliki hisa chache kuelekea Dira 2050

Na Mwandishi wetu, Arusha SERIKALI imetoa maelekezo nane ya kimkakati yanayolenga kuimarisha utendaji wa kampuni...

More like this

Yanga kuikabili TRA bila Depu, kocha aeleza ugumu ulipo

Na Mwandishi Wetu WAKATI Yanga ikitarajiwa kushuka dimbani kesho Machi 18, 2026  kuikabili TRA United katika Ligi...

Vijana 3,967 waomba uwezeshaji kupitia Go Green na IMBEJU ya CRDB Bank Foundation

Na Mwandishi wetu JUMLA ya vijana 3,967 kutoka maeneo mbalimbali nchini wamewasilisha maombi ya...

RC Kunenge aipongeza Dawasa, awapa jukumu madiwani

Na Mwandishi wetu MKUU wa Mkoa wa Pwani, Abubakar Kunenge amesema ushirikishwaji wananchi kwenye...