Mkurugenzi Mkuu NIRC atoa pole kwa waandishi wa habari waliopata ajali Iringa

Na Mwandishi Wetu

MKURUGENZI Mkuu wa Tume ya Taifa ya Umwagiliaji (NIRC), Raymond Mndolwa, ametoa pole kwa waandishi wa habari waliopata ajali ya gari mkoani Iringa walipokuwa wakirejea nyumbani wakitokea kuripoti Maadhimisho ya Miaka 49 ya Chama Cha Mapinduzi (CCM).

Mndolwa, akiwa ameambatana na Mkuu wa Kitengo cha Habari na Mawasiliano wa NIRC, Mariam Mziwanda, alifika katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Iringa na kuwatembelea waandishi hao wa habari, ambapo aliwajulia hali na kuwapa pole kwa niaba ya taasisi hiyo.

Ajali hiyo ilitokea jana, Februari 5, 2026, katika Kata ya Idodi, Wilaya ya Iringa Vijijini.

Gari lililohusika katika ajali hiyo lilikuwa limewabeba Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM Mkoa wa Iringa, Joseph Nzala Lyata, pamoja na waandishi wa habari akiwemo Frank Leonard, Mwenyekiti wa Chama cha Waandishi wa Habari Mkoa wa Iringa na mwandishi wa magazeti ya Habari Leo na Daily News.

Waandishi wengine waliopata ajali hiyo ni pamoja na Zuhura Zukheriwa wa Abood TV, Denis Mlowe wa blogu ya Fullshangwe, Clemence Sanga wa Channel Ten pamoja na Herieth Mola wa Mkombozi Online TV.

spot_img

Latest articles

Baraza la wafanyakazi Siri ya utendaji bora

Na Mwandishi Wetu BARAZA la Wafanyakazi la Sita la TMDA limefanyika kwa ufanisi tarehe...

Baraza la sita la wafanyakazi lachagiza mafanikio ya TMDA

Na Mwandishi Wetu MKURUGENZI Mkuu wa TMDA, Dkt. Adam Fimbo, ametoa pongezi kwa wajumbe...

TMA yatoa mwelekeo wa mvua za Masika Machi hadi Mei 2026

Na Tatu Mohamed  MAMLAKA ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) imetoa mwelekeo wa mvua za...

Simba yataka Polisi iwashughulikie waliomkashfu bosi

Na Mwandishi Wetu KLABU ya Simba imeliandikia barua Jeshi la Polisi  ili kuwachukulia...

More like this

Baraza la wafanyakazi Siri ya utendaji bora

Na Mwandishi Wetu BARAZA la Wafanyakazi la Sita la TMDA limefanyika kwa ufanisi tarehe...

Baraza la sita la wafanyakazi lachagiza mafanikio ya TMDA

Na Mwandishi Wetu MKURUGENZI Mkuu wa TMDA, Dkt. Adam Fimbo, ametoa pongezi kwa wajumbe...

TMA yatoa mwelekeo wa mvua za Masika Machi hadi Mei 2026

Na Tatu Mohamed  MAMLAKA ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) imetoa mwelekeo wa mvua za...