Kipa wa zamani Yanga afariki dunia

Na Winfrida Mtoi

KIPA wa zamani wa Yanga na timu ya Taifa ya Tanzania, Peter Manyika amefariki dunia leo Januari 26, 2025, wakati akiwa anapatiwa matibabu katika hospitali ya St. Monica, jijini Dar es Salaam.

Familia kupitia mtoto wake, Manyika JR imethibitisha kuwa baba yake amefariki, mwili umehifadhiwa katika hospitali ya Mwananyamala, na msiba upo nyumbani kwao Mbezi.

Manyika atakumbukwa katika historia ya soka nchini kama miongoni mwa makipa bora waliojipatia heshima kubwa nchini akiwa na Yanga na timu ya Taifa kuanzia miaka ya mwishoni mwa miaka ya 1980 na 1990.

Mwaka 1999 aliiongoza Yanga kutwaa ubingwa wa Kombe la Klabu Bingwa Afrika Mashariki na Kati mwaka 1999 nchini Uganda.

Baada ya kustaafu soka la ushindani, hakuachana na mchezo huo, aliamua kujikita katika ukocha wa makipa na kuendeleza vipaji, akifanya kazi na klabu  mbalimbali zikiwamo Ihefu, Fountain Gate na timu za taifa za vijana.

Mwaka 2019 klabu yake za zamani, Yanga ilimpa jukumu la kuwanoa makipa wa timu hiyo akichukua nafasi ya Juma Pondamali, kipindi hicho alikuwa ni Metecha Mnata, Faroukh Shikalo, Klaus Kindoki na Ramadhan Kabwili.

spot_img

Latest articles

JAB yazindua mwongozo wa kisheria wa utoaji wa Ithibati ya maisha kwa waandishi

Na Mwandishi Wetu BODI ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imezindua rasmi Mwongozo wa...

BRELA YAIBUA FURSA MPYA ULINZI WA ALAMA ZA BIASHARA KWA WAJASIRIAMALI

Na Mwandishi Wetu Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA) imewataka wajasiriamali wanaoshiriki...

TTB yakutanisha wadau kujadili mustakabali wa Destination Tanzania

Na Mwandishi Wetu Bodi ya Utalii Tanzania (TTB) imewakutanisha wadau mbalimbali wa sekta ya...

Dkt. Jafar Seif: Banda la Ofisi ya Waziri Mkuu Sabasaba larahisisha upatikanaji wa huduma kwa wananchi

Na Mwandishi Wetu NAIBU Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu – Tawala za...

More like this

JAB yazindua mwongozo wa kisheria wa utoaji wa Ithibati ya maisha kwa waandishi

Na Mwandishi Wetu BODI ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imezindua rasmi Mwongozo wa...

BRELA YAIBUA FURSA MPYA ULINZI WA ALAMA ZA BIASHARA KWA WAJASIRIAMALI

Na Mwandishi Wetu Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA) imewataka wajasiriamali wanaoshiriki...

TTB yakutanisha wadau kujadili mustakabali wa Destination Tanzania

Na Mwandishi Wetu Bodi ya Utalii Tanzania (TTB) imewakutanisha wadau mbalimbali wa sekta ya...