Yanga bingwa Mapinduzi Cup 2026

Na Mwandishi Wetu

YANGA imetwaa ubingwa wa kombe la Mapinduzi ikiifunga Azam FC kwa mikwaju ya penalti 5-4 katika mchezo wa fainali uliopigwa Januari 13, 2026 kwenye dimba la Gombani, Pemba.

Mchezo huo uliishia kwa sare tasa ndani ya dakika 90 za kawaida, hali iliyomlazimu mwamuzi kuongeza muda wa nyingeza dakika 30 ili kumpata mshindi, lakini hakuna timu iliyofanikiwa kufunga.

Katika dakika ya 115 ya mchezo, Yanga ilipata penalti lakini kipa wa Azam Aishi Manula aliokoa mkwaju huo uliopigwa na Pacôme Zouzoua, huku Azam ikiwa pungufu.

Mchezo huo ulikuwa ni mgumu kwa pande zote, licha ya Azam kucheza pungufu tangu dakika ya 74 baada ya mchezaji wao Cheikna Diakite kuoneshwa kadi nyekundu.

Aidha Max Nzengeli wa Yanga amekiwa mchezaji bora wa mashindano (MVP), Manula kipa bora na Jephte Kitambala wa Azam akiibuka mfungaji bora.

spot_img

Latest articles

JAB yazindua mwongozo wa kisheria wa utoaji wa Ithibati ya maisha kwa waandishi

Na Mwandishi Wetu BODI ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imezindua rasmi Mwongozo wa...

BRELA YAIBUA FURSA MPYA ULINZI WA ALAMA ZA BIASHARA KWA WAJASIRIAMALI

Na Mwandishi Wetu Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA) imewataka wajasiriamali wanaoshiriki...

TTB yakutanisha wadau kujadili mustakabali wa Destination Tanzania

Na Mwandishi Wetu Bodi ya Utalii Tanzania (TTB) imewakutanisha wadau mbalimbali wa sekta ya...

Dkt. Jafar Seif: Banda la Ofisi ya Waziri Mkuu Sabasaba larahisisha upatikanaji wa huduma kwa wananchi

Na Mwandishi Wetu NAIBU Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu – Tawala za...

More like this

JAB yazindua mwongozo wa kisheria wa utoaji wa Ithibati ya maisha kwa waandishi

Na Mwandishi Wetu BODI ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imezindua rasmi Mwongozo wa...

BRELA YAIBUA FURSA MPYA ULINZI WA ALAMA ZA BIASHARA KWA WAJASIRIAMALI

Na Mwandishi Wetu Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA) imewataka wajasiriamali wanaoshiriki...

TTB yakutanisha wadau kujadili mustakabali wa Destination Tanzania

Na Mwandishi Wetu Bodi ya Utalii Tanzania (TTB) imewakutanisha wadau mbalimbali wa sekta ya...