Mwakinyo ashinda kwa K.O, afichua siri

Na Winfrida Mtoi

Bondia wa ngumi za kulipwa nchini, Hassan Mwakinyo ameibuka mshindi kwa K.O dhidi ya mpinzani wake Stanley Eribo kutoka Nigeria, baada ya kumaliza pambano katika raundi mbili.

Pambano hilo limemalizika usiku huu katika ukumbi wa Warehouse Masaki, jijini Dar es Salaam.

Akizungumzia pambano hilo, Mwakinyo amesema imekuwa rahisi kwake kumshinda mpinzani wake kutokana na mazoezi anayofanya bila kujali ana mchezo au hana.

Amesema ubora wake haushuki hata akikaa muda mrefu bila kucheza kwa kuwa ameweka heshima katika mazoezi na anaamini ndiyo mhimili wa kazi yake.

Katika pambano lingine Mtanzania Hamadi Furahisha ameibuka mshindi kwa pointi dhidi ya Mmalawi Hanock Phiri katika pambano la raundi 10, huku Hassan Ndonga akimchapa Ismail Boyka.

spot_img

Latest articles

Mwakinyo kuilipia kisasi Taifa Stars dhidi ya Mnigeria kesho, Furahi apania rekodi

Na Winfrida Mtoi BONDIA wa kimataifa wa Tanzania, Hassan Mwakinyo, ameweka bayana kuwa pambano lake...

Serikali kuendelea kuwawezesha vijana kijamii, kiuchumi

Na Tatu Mohamed WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Rais – Maendeleo ya Vijana, Joel...

Kids Holiday Festival yawavuta mamia ya watoto, CRDB yatumia jukwaa kujenga uelewa wa fedha

Na Mwandishi Wetu BURUDANI na michezo mbalimbali vilitawala Tamasha la Kids Holiday Festival lililowakusanya...

Mambo: Demokrasia haijengwi kwa mashinikizo, vitisho

Na Mwandishi Wetu ALIYEKUWA Mgombea wa Bavicha Taifa, Masoud Mambo amesema kuwa demokrasia ya...

More like this

Mwakinyo kuilipia kisasi Taifa Stars dhidi ya Mnigeria kesho, Furahi apania rekodi

Na Winfrida Mtoi BONDIA wa kimataifa wa Tanzania, Hassan Mwakinyo, ameweka bayana kuwa pambano lake...

Serikali kuendelea kuwawezesha vijana kijamii, kiuchumi

Na Tatu Mohamed WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Rais – Maendeleo ya Vijana, Joel...

Kids Holiday Festival yawavuta mamia ya watoto, CRDB yatumia jukwaa kujenga uelewa wa fedha

Na Mwandishi Wetu BURUDANI na michezo mbalimbali vilitawala Tamasha la Kids Holiday Festival lililowakusanya...