Mavazi ya kitamaduni kivutio kingine AFCON 2025

Na Winfrida Mtoi

SHAMRASHAMRA kuelekea Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON-2025), zimezidi kupamba moto, hasa baada ya timu shiriki za michuano hiyo kuanza kuwasili nchini Morocco ambako yatafanyika mashindano hayo makubwa ya soka barani Afrika.

Mashindano hayo yayonatarajiwa kuanza Jumapili Desemba 21, 2025, yakishirikisha mataifa 24, yamekuwa kama fursa ya kipekee kwa baadhi ya nchi za Afrika kuonyesha utajiri wa tamaduni zao kupitia mavazi ya asili.

Kutokana na hilo mashindano hayo yanaonekana si kuhusu mpira pekee bali kuna vionjo vingi vinavyoyamba. Mashabiki wamekuwa wakivutiwa na hali hiyo, kwa mfano ukiangalia  jinsi  mataifa  mbalimbali kama vile Nigeria, Senegal, Mali, Benin  na Comoro walivyowasili Morocco ambapo wachezaji wao wameonekana wakiwa wamevalia mavazi ya kitamaduni.

Hivyo aina hiyo ya mavazi inaonekana si urembo pekee bali ni utambulisho kimataifa unaoboresha taswira na sifa ya nchi, hali inayosaidia kuvutia watalii.

Afrika Magharibi wameonekana kuwa wazuri zaidi katika ubunifu wa mavazi yao ya kitamaduni  tofauti nan chi nyingine kama Tanzania, Zambia, Afrika Kusini, Angola na wengine ambao timu zao zimewasili zikiwa katika mavazi ya kawaida ya kimichezo.

Fainali hizo zinatarajiwa kuanza Jumapili Desemba 21, 2025, jumla ya mataifa 24 yakichuana ikiwamo Tanzania.

spot_img

Latest articles

ETDCO yaahidi kukamilisha Mradi wa Umeme katika vitongoji 372 Ruvuma kwa wakati

Na Mwandishi Wetu KAMPUNI ya Ujenzi na Ukarabati wa Miundombinu ya Usafirishaji na Usambazaji...

Wadau sekta ya Hali ya Hewa wajadili utabiri wa Masika 2026

Na Mwandishi Wetu WADAU kutoka sekta mbalimbali nchini wamekutana kujadili utabiri wa msimu wa...

WMA yafunga Mtambo wa kisasa unaohakiki Dira za Maji Dodoma

Na Mwandishi Wetu WAKALA wa Vipimo (WMA) umesimika mtambo wa kisasa wa kidijitali wa...

Benki ya CRDB yaja na ‘Benki Kimpango Wako’ yaahidi huduma bora zaidi mwaka 2026

Na Mwandishi wetu BENKI ya CRDB imezindua kampeni yake ya mwaka 2026 inayoitwa ‘Benki Kimpango...

More like this

ETDCO yaahidi kukamilisha Mradi wa Umeme katika vitongoji 372 Ruvuma kwa wakati

Na Mwandishi Wetu KAMPUNI ya Ujenzi na Ukarabati wa Miundombinu ya Usafirishaji na Usambazaji...

Wadau sekta ya Hali ya Hewa wajadili utabiri wa Masika 2026

Na Mwandishi Wetu WADAU kutoka sekta mbalimbali nchini wamekutana kujadili utabiri wa msimu wa...

WMA yafunga Mtambo wa kisasa unaohakiki Dira za Maji Dodoma

Na Mwandishi Wetu WAKALA wa Vipimo (WMA) umesimika mtambo wa kisasa wa kidijitali wa...