Taifa Stars yakabidhiwa bendera tayari kwa AFCON 2025

Na Mwandishi Wetu

WAZIRI wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Prof. Palamagamba Kabudi, ameiaga na kuikabidhi bendera timu ya Taifa ya Tanzania, Taifa Stars kuelekea fainali za Mataifa ya Afrika (AFCON 2025).

Hafla hiyo imefanyika nchini Misri ambako Taifa Stars ilikuwa kambini kujiandaa na mashindano hayo, kabla ya timu kuelekea Morocco kwa michuano hiyo inayotarajia kuanza Desemba 21.

Akizungumza wakati wa halfa hiyo, Prof. Kabudi, amekiahidi kikosi hicho ushirikiano wa kila aina katika kuhakikisha kikosi hicho kinafanya vyema katika michuano hiyo mikubwa na yenye heshima kubwa barani Afrika na  duniani kwa ujumla.

Aidha  amewahimiza Watanzania kuipenda na kuipa moyo timu yao ya Stars kwa kuwashangilia na wale watakao kuwa na nafasi kwenda kujiunga nao kwenye mechi zao zote watakazocheza huko nchini Morocco.

Katika michuano hiyo Taifa Stars ipo kundi C lenye timu za Nigeria, Tunisia na Uganda, ambapo kikosi hicho kinachonolewa na kocha Miguel Gamondi  mchezo wa kwanza kitakutana na Nigeria Desemba 21, 2025 Uwanja wa Fès Sports Complex, Morocco

spot_img

Latest articles

Polisi yachunguza tukio la kuchoma moto magari msibani

Na Mwandishi Wetu JESHI la Polisi Mkoa wa Morogoro limesema linachunguza tukio la kuchoma moto na...

CRDB yashirikiana na Kids’ Holiday Festival kukuza elimu ya fedha kwa watoto

Na Mwandishi Wetu BENKI ya CRDB imeingia makubaliano ya ushirikiano na Kids’ Holiday Festival...

Katibu Mkuu Kiongozi awataka maofisa habari serikalini kujiimarisha kiutendaji kukabiliana na teknolojia

Na Winfrida Mtoi KATIBU Mkuu Kiongozi, Balozi Dk. Moses Kusiluka amewataka Maofisa Habari wa Serikali...

More like this

Polisi yachunguza tukio la kuchoma moto magari msibani

Na Mwandishi Wetu JESHI la Polisi Mkoa wa Morogoro limesema linachunguza tukio la kuchoma moto na...

CRDB yashirikiana na Kids’ Holiday Festival kukuza elimu ya fedha kwa watoto

Na Mwandishi Wetu BENKI ya CRDB imeingia makubaliano ya ushirikiano na Kids’ Holiday Festival...

Katibu Mkuu Kiongozi awataka maofisa habari serikalini kujiimarisha kiutendaji kukabiliana na teknolojia

Na Winfrida Mtoi KATIBU Mkuu Kiongozi, Balozi Dk. Moses Kusiluka amewataka Maofisa Habari wa Serikali...