Chuo cha Malya chawafunda wakufunzi wa gym

Na Winfrida Mtoi

CHUO cha Maendeleo ya Michezo Malya kinaendesha mafunzo maalum kwa wakufunzi wa gym  na makocha wa viungo ili kuwaongezea ujuzi na  kufahamu mbinu mbalimbali zitakazowasaidia kufanya kazi yao kwa weledi.

Mafunzo hayo yaliyoanza Novemba 24,2025 yanayoendelea katika ukumbi wa Uwanja wa Mkapa, jijini Dar es Salaam, yanahusisha washiriki 30 kutoka mikoa mbalimbali ya Tanzania.

Akizungumzia lengo la kutoa mafunzo hayo, Makamu wa Mwenyekiti wa Chuo hicho, Salumu Mtumbuka amesema ni kutokana na kukua kwa michezo na  maeneo ya gym ndiyo watu wengi wanapenda kwenda kufanya mazoezi.

“Tumeona tutoe mafunzo haya kwa makocha  wa viungo wa michezo yote na wataalamu wa  gmy ambao wanafundisha watu kufanya mazoezi,  hii itasaidia kutoa elimu yao kitaalamu zaidi.

“Tutaendelea kutoa mafunzo ya michezo kwa lengo ya kupata wataalum ambao wataleta maendeleo katika Taifa letu, pia nina imani elimu hii ambayo washiriki wanapatiwa itaongeza nguvu katika mazoezi yao, “ameeleza.

Kwa upande wake mshiriki wa mafunzo hayo, Peter Pingo amesema elimu aliyoipata itamuongezea ubora katika kazi yake ya kufundisha mazoezi gym.

“Naishukuru Serikali chini ya Chuo ya Malya ambao wametoa kozi hii ambayo itatuongezea weledi na ufanisi wa kazi yetu, nina imani nitakuwa bora zaidi katika kuhakikisha watu wanapata mazoezi yenye viwango vizuri, ” ameeleza.

spot_img

Latest articles

Tanesco yagusa mioyo ya watoto wenye mahitaji maalum

📌Ni sehemu ya uwajibikaji wake kwa jamii 📌Yatoa misaada mbalimbali kwa vituo vitatu Dar...

 ‘Umimi’ wa viongozi unaua Jumuiya Afrika Mashariki

KATIKATI ya miaka ya 90 wakati mfumo wa vyama vingi unaota mizizi, lilitokea wazo...

Wanafunzi watatu wafariki dunia baada ya kupigwa na radi Dar

Na Mwandishi wetu WANAFUNZI watatu wa Shule ya Msingi Msongola iliyopo eneo la Msongola,...

Serikali yawataka Wakurugenzi kuongeza thamani inayopimika katika uwekezaji wa hisa chache

Na Mwandishi wetu SERIKALI imewataka wakurugenzi wa bodi za kampuni ambazo ina umiliki wa...

More like this

Tanesco yagusa mioyo ya watoto wenye mahitaji maalum

📌Ni sehemu ya uwajibikaji wake kwa jamii 📌Yatoa misaada mbalimbali kwa vituo vitatu Dar...

 ‘Umimi’ wa viongozi unaua Jumuiya Afrika Mashariki

KATIKATI ya miaka ya 90 wakati mfumo wa vyama vingi unaota mizizi, lilitokea wazo...

Wanafunzi watatu wafariki dunia baada ya kupigwa na radi Dar

Na Mwandishi wetu WANAFUNZI watatu wa Shule ya Msingi Msongola iliyopo eneo la Msongola,...