Bondia Mrembo apewa Mmalawi

Na Mwandishi Wetu

BONDIA Debora Mwenda maarufu Bondia Mrembo, ameahidi kuiwakilisha vizuri Tanzania dhidi ya Mariam Dick kutoka Malawi watakapokutana katika pambano la Box on Boxing Day Desemba 26,2025, Warehouse Masaki Dar es Salaam.

Akizungumza leo Novemba 26, 2025, Debora amesema itakuwa  mara yake ya kwanza  kucheza pambano la kimataifa lakini anawaahidi watanzamia kuonesha mchezo mzuri na kuibuka na ushindi wa kishindo.

“Nashukuru kwa nafasi hii niliyoipata, ya kuonesha kitu nilichonacho, nimejiandaa vyakutosha nataka kuwaonesha watanzania kuwa najua kuufanya mchezo huu hata zaidi ya mwanaume,”

Amesema hana woga wowote kwa sababu amewekeza nguvu zake zaidi katika mazoezi na kila siku zinavyokwenda anazidi kuwa bora.

‎Naye mwalimu wa bondia huyo, Dickson Tembo amesema, anaendelea na mazoezi ya kibabe,hivyo watanzania wajiandae kushangilia ushindi wa kishindo siku hiyo.

spot_img

Latest articles

Uwanja wa Mkwakwani wafungiwa

Na Mwandishi Wetu SHIRIKISHO la Soka Tanzania (TFF), limeufungia Uwanja wa Mkwakwani, Tanga kutumika kwa...

Tuzo za TFF za msimu wa 2024/25 zayeyuka

Na Mwandishi Wetu Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) limetoa taarifa ya kuahirisha hafla ya utoaji...

Chuo cha Malya chawafunda wakufunzi wa gym

Na Winfrida Mtoi CHUO cha Maendeleo ya Michezo Malya kinaendesha mafunzo maalum kwa wakufunzi wa...

Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, Ikulu  ajiuzulu TEF

Na Mwandishi Wetu MKURUGENZI wa Mawasiliano ya Rais, Ikulu, Bakari Machumu amejiuzulu nafasi ya makamu...

More like this

Uwanja wa Mkwakwani wafungiwa

Na Mwandishi Wetu SHIRIKISHO la Soka Tanzania (TFF), limeufungia Uwanja wa Mkwakwani, Tanga kutumika kwa...

Tuzo za TFF za msimu wa 2024/25 zayeyuka

Na Mwandishi Wetu Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) limetoa taarifa ya kuahirisha hafla ya utoaji...

Chuo cha Malya chawafunda wakufunzi wa gym

Na Winfrida Mtoi CHUO cha Maendeleo ya Michezo Malya kinaendesha mafunzo maalum kwa wakufunzi wa...