Naibu Waziri Nishati, akutana na Menejimenti ya Ewura, aitaka kuongeza kasi na ufanisi zaidi

Na Mwandishi Wetu

NAIBU Waziri wa Nishati, Salome Makamba, leo tarehe 24.11.2025 amekutana na Menejimenti ya Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA), ikiwa ni mara ya kwanza tangu kuteuliwa katika nafasi hiyo hivi karibuni.

Makamba amekutana na viongozi hao kwa lengo la kujadiliana masuala mbalimbali ya utendaji na maboresho ya sekta ya nishati nchini.

Mkutano huo umefanyika katika Ofisi za Makao Makuu ya EWURA jijini Dodoma.

Aidha, ameipongeza EWURA kwa kazi nzuri katika kusimamia huduma za nishati, na kuitaka Mamlaka hiyo kuongeza kasi, ubunifu na ufanisi.

“Mimi si muumini wa kushindwa, hivyo natoa rai kwenu kujipanga ili kuendana na kasi hiyo, ili muendelee kung’ara katika uendeshaji wa shughuli zenu” alisema.

Mkurugenzi Mkuu wa EWURA, Dkt. James Andilile, aliwasilisha mbele ya Makamba taarifa fupi kuhusu majukumu ya Mamlaka, mafanikio yaliyopatikana, pamoja na maeneo yanayoendelea kuimarishwa.

Dkt. Andilile aliahidi taasisi yake kuongeza ufanisi katika utekelezaji wa majukumu yake ili kuhakikisha wananchi wanapata huduma bora, salama na za uhakika.

spot_img

Latest articles

DCEA yateketeza kilo 504.36 za Heroin Mtwara

Na Mwandishi Wetu, Mtwara MAMLAKa ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya (DCEA) imeteketeza...

Mkurugenzi wa Rasilimali Watu Tanesco awahakikishia ushirikiano maafisa huduma kwa wateja

📌 Afunga Mkutano Mkuu wa Mwaka wa Maafisa hao 📌 Awapongeza kwa utendaji bora wenye...

Makonda  awajibu wanaoponda ziara ya Rio

Na Winfrida Mtoi WAZIRI wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Paul Makonda amesema ziara ya...

TIRDO yasajili Viwanda 25,650, Yaongeza Maabara za Kisasa Kuimarisha Sekta ya Viwanda

Na Mwandishi Wetu WIZARA ya Viwanda na Biashara kupitia Shirika la Utafiti na Maendeleo ya...

More like this

DCEA yateketeza kilo 504.36 za Heroin Mtwara

Na Mwandishi Wetu, Mtwara MAMLAKa ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya (DCEA) imeteketeza...

Mkurugenzi wa Rasilimali Watu Tanesco awahakikishia ushirikiano maafisa huduma kwa wateja

📌 Afunga Mkutano Mkuu wa Mwaka wa Maafisa hao 📌 Awapongeza kwa utendaji bora wenye...

Makonda  awajibu wanaoponda ziara ya Rio

Na Winfrida Mtoi WAZIRI wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Paul Makonda amesema ziara ya...