Simba yaachia pointi tatu kwa Mkapa, Azam nayo mambo magumu

Na Winfrida Mtoi

Simba imeshindwa kutamba nyumbani baada ya kufungwa na Petro de Luanda bao 1-0 kwenye Uwanja wa Benjamin Mkapa, jijjni Dar es Salaam.

Matokeo hayo yamewafanya mashabiki wa timu hiyo waliojitokeza kwa wingi kuondoka kwa unyonge uwanjani wakiwa hawaamini kilichotokea.

Wikiendi ijayo Simba itakuwa ugenini nchini Mali kuikabili Stade Malien ambayo jana ilitoka suluhu na Esperance ya Tunisia.


Wawakilishi wengine wa Tanzania katika Kombe la Shirikisho Afrika, Azam FC wameanza vibaya hatua ya makundi ya michuano hiyo kwa kufungwa ugenini mabao 2-0 na AS Maniema ya DR Congo.

Kati ya wawakilishi wanne wa Tanzania katika michuano hiyo ya CAF yaani Ligi ya Mabingwa Afrika na Kombe la. Shirikisho, Yanga pekee ndio imeanza vizuri kwa ushindi wa bao 1-0 dhidi ya FAR Rabat ya Morocco, wakati Singida Bs ikipoteza ugenini kwa kufungwa 2-0 na CR Belouizdad

spot_img

Latest articles

ETDCO yaahidi kukamilisha Mradi wa Umeme katika vitongoji 372 Ruvuma kwa wakati

Na Mwandishi Wetu KAMPUNI ya Ujenzi na Ukarabati wa Miundombinu ya Usafirishaji na Usambazaji...

Wadau sekta ya Hali ya Hewa wajadili utabiri wa Masika 2026

Na Mwandishi Wetu WADAU kutoka sekta mbalimbali nchini wamekutana kujadili utabiri wa msimu wa...

WMA yafunga Mtambo wa kisasa unaohakiki Dira za Maji Dodoma

Na Mwandishi Wetu WAKALA wa Vipimo (WMA) umesimika mtambo wa kisasa wa kidijitali wa...

Benki ya CRDB yaja na ‘Benki Kimpango Wako’ yaahidi huduma bora zaidi mwaka 2026

Na Mwandishi wetu BENKI ya CRDB imezindua kampeni yake ya mwaka 2026 inayoitwa ‘Benki Kimpango...

More like this

ETDCO yaahidi kukamilisha Mradi wa Umeme katika vitongoji 372 Ruvuma kwa wakati

Na Mwandishi Wetu KAMPUNI ya Ujenzi na Ukarabati wa Miundombinu ya Usafirishaji na Usambazaji...

Wadau sekta ya Hali ya Hewa wajadili utabiri wa Masika 2026

Na Mwandishi Wetu WADAU kutoka sekta mbalimbali nchini wamekutana kujadili utabiri wa msimu wa...

WMA yafunga Mtambo wa kisasa unaohakiki Dira za Maji Dodoma

Na Mwandishi Wetu WAKALA wa Vipimo (WMA) umesimika mtambo wa kisasa wa kidijitali wa...