Sababu za kiusalama zazuia Lissu kufikishwa mahakamani

Na Mwandishi Wetu

Jeshi la Magereza limeshindwa kumfikisha mahakamani Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Tundu Lissu, anayekabiliwa na kesi ya uhaini, kutokana na sababu za kiusalama.

Leo Novemba 10, 2025 Lissu alitarajiwa kufikishwa  katika Mahakama Kuu, Masjala Ndogo ya Dar es Salaam mbele ya jopo la majaji watatu wa Mahakama Kuu, wakiongozwa na Jaji Dunstan Ndunguru, wakisaidiwa na Majaji James Karayemaha na Ferdinand Kiwonde, kwa ajili ya kusikilizwa kwa shahidi wa nne wa upande wa Jamhuri kutoa ushahidi wake dhidi ya kiongozi huyo wa Chadema.

Wakili wa Serikali Mwandamizi, Thawabu Issa, aliieleza mahakama kuwa walifika mahakamani na  kugundua kwamba mshtakiwa hakuwepo, hivyo kufanya  jitihada za kuwasiliana na Mkuu wa Gereza kujua sababu za kutokuwepo kwake.

“Tulipofika hapa tulikuta mshtakiwa hayupo. Tulifanya jitihada za kuwasiliana na Mkuu wa Gereza na tukaelezwa kwamba wameshindwa kumfikisha kwa sababu za kiusalama,” amesema Wakili Issa.

Upande wa Jamhuri uliiomba Mahakama kuhairisha kesi hiyo kwa siku 14, lakini katika maamuzi yake Mahakama kupitia Jaji Danstan Ndunguru ikatoa maelekezo kuwa shauri hilo linaahirishwa hadi Jumatano na si kwa siku 14 kama ilivyoombwa na Jamhuri. Huku akisisitiza  kuwa mshtakiwa  pamoja na wafikishwe makahamani ili shauri liendelee.

spot_img

Latest articles

DCEA yateketeza kilo 504.36 za Heroin Mtwara

Na Mwandishi Wetu, Mtwara MAMLAKa ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya (DCEA) imeteketeza...

Mkurugenzi wa Rasilimali Watu Tanesco awahakikishia ushirikiano maafisa huduma kwa wateja

📌 Afunga Mkutano Mkuu wa Mwaka wa Maafisa hao 📌 Awapongeza kwa utendaji bora wenye...

Makonda  awajibu wanaoponda ziara ya Rio

Na Winfrida Mtoi WAZIRI wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Paul Makonda amesema ziara ya...

TIRDO yasajili Viwanda 25,650, Yaongeza Maabara za Kisasa Kuimarisha Sekta ya Viwanda

Na Mwandishi Wetu WIZARA ya Viwanda na Biashara kupitia Shirika la Utafiti na Maendeleo ya...

More like this

DCEA yateketeza kilo 504.36 za Heroin Mtwara

Na Mwandishi Wetu, Mtwara MAMLAKa ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya (DCEA) imeteketeza...

Mkurugenzi wa Rasilimali Watu Tanesco awahakikishia ushirikiano maafisa huduma kwa wateja

📌 Afunga Mkutano Mkuu wa Mwaka wa Maafisa hao 📌 Awapongeza kwa utendaji bora wenye...

Makonda  awajibu wanaoponda ziara ya Rio

Na Winfrida Mtoi WAZIRI wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Paul Makonda amesema ziara ya...