Rasmi Kocha Yanga afungashiwa virago usiku

Na Mwandishi Wetu

Uongozi wa Klabu ya Yanga umevunja mkataba na Kocha Mkuu, Romain Folz.

Uamuzi huo umekuja saa chache baada ya kupoteza mchezo kwa kufungwa ugenini na Silver Strikers bao 1-0 katika mchezo wa Ligi ya Mabingwa Afrika.

Kwa mujibu wa taarifa ya klabu hiyo iliyotolewa usiku huu, timu itakuwa chini ya Kocha Msaidizi Patrick Mabedi, huku mchakato wa kumtafuta mwingine ukiendelea.

Folz raia wa Ufaransa alijiunga na Wanajangwani hao, Julai, 2025 akitokea klabu ya Olympique Akbou ya Algeria ambako alikuwa Mkurugenzi wa Ufundi.

Kocha Romuald Rakotondrabe kutoka Madagascar anatajwa kuwa ndiye atakayechukua nafasi ya Mfaransa huyo.

spot_img

Latest articles

Mwanamke ashikiliwa  Polisi kwa  kumuua mume wake na kumfukia ndani ya nyumba yao

Na Mwandishi Wetu Jeshi la Polisi Mkoa wa Geita linamshikilia mwanamke mmoja aliyefahamika kwa jina...

Padre aliyepotea apatikana akiwa hai

Na Mwandishi Wetu Jeshi la Polisi mkoani Ruvuma limefanikiwa kumpata Padre Camillus Nikata wa Jimbo...

Waangalizi wa Uchaguzi watakiwa kutoingilia mchakato wa Uchaguzi Mkuu

Na Mwandishi wetu, Dodoma WAANGALIZI wa Uchaguzi wa ndani na wa kimataifa wametakiwa kuzingatia sheria...

More like this

Mwanamke ashikiliwa  Polisi kwa  kumuua mume wake na kumfukia ndani ya nyumba yao

Na Mwandishi Wetu Jeshi la Polisi Mkoa wa Geita linamshikilia mwanamke mmoja aliyefahamika kwa jina...

Padre aliyepotea apatikana akiwa hai

Na Mwandishi Wetu Jeshi la Polisi mkoani Ruvuma limefanikiwa kumpata Padre Camillus Nikata wa Jimbo...