Padre aliyepotea apatikana akiwa hai

Na Mwandishi Wetu

Jeshi la Polisi mkoani Ruvuma limefanikiwa kumpata Padre Camillus Nikata wa Jimbo Kuu la Songea, ambaye pia ni Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augustino Tanzania (SAUT) – Mwanza, aliyeripotiwa kupotea mnamo Oktoba 09, 2025.

Akizungumza na waandishi wa habari leo Oktoba 17,2025  Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Ruvuma, Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi, Marco  Chilya, amesema Padre huyo hakutekwa kama ambavyo ilidhaniwa bali alijipoteza kutokana na sababu za msongo wa mawazo.

Kamanda huyo ameeleza kuwa Padre amepatikana akiwa hai katika mashamba ya Kijiji cha Mawa, kilichopo Kata ya Hanga, Wilaya ya Namtumbo ambapo ni nyumbani kwao.

Aidha ameongeza kuwa Padre huyo alikutwa akiwa  amedhoofika kwa njaa huku akiwa na begi dogo la mgongoni ambalo lilikuwa na taulo alilokuwa akitumia kulalia, hati yake ya kusafiria, karanga alizokuwa akitumia kama chakula, maji, funguo ya chumba alichokuwa akitumia kabla ya jimboni kwake, fedha taslimu kiasi cha Shilingi 13,500, saa ya mkononi, simu ya mkononi akiwa ameizima  pamoja na dawa za  maumivu.

Ameeleza kuwa  kwa sasa Padre huyo amelazwa katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Songea (Homso) akiendelea na matibabu kutokana na kudhoofika kwa afya yake.

spot_img

Latest articles

JAB yazindua mwongozo wa kisheria wa utoaji wa Ithibati ya maisha kwa waandishi

Na Mwandishi Wetu BODI ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imezindua rasmi Mwongozo wa...

BRELA YAIBUA FURSA MPYA ULINZI WA ALAMA ZA BIASHARA KWA WAJASIRIAMALI

Na Mwandishi Wetu Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA) imewataka wajasiriamali wanaoshiriki...

TTB yakutanisha wadau kujadili mustakabali wa Destination Tanzania

Na Mwandishi Wetu Bodi ya Utalii Tanzania (TTB) imewakutanisha wadau mbalimbali wa sekta ya...

Dkt. Jafar Seif: Banda la Ofisi ya Waziri Mkuu Sabasaba larahisisha upatikanaji wa huduma kwa wananchi

Na Mwandishi Wetu NAIBU Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu – Tawala za...

More like this

JAB yazindua mwongozo wa kisheria wa utoaji wa Ithibati ya maisha kwa waandishi

Na Mwandishi Wetu BODI ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imezindua rasmi Mwongozo wa...

BRELA YAIBUA FURSA MPYA ULINZI WA ALAMA ZA BIASHARA KWA WAJASIRIAMALI

Na Mwandishi Wetu Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA) imewataka wajasiriamali wanaoshiriki...

TTB yakutanisha wadau kujadili mustakabali wa Destination Tanzania

Na Mwandishi Wetu Bodi ya Utalii Tanzania (TTB) imewakutanisha wadau mbalimbali wa sekta ya...