Mwanamke ashikiliwa  Polisi kwa  kumuua mume wake na kumfukia ndani ya nyumba yao

Na Mwandishi Wetu

Jeshi la Polisi Mkoa wa Geita linamshikilia mwanamke mmoja aliyefahamika kwa jina la Matha Japheth (44), kabila ni Mnyamwezi , Mkulima Mkazi wa Kitongoji cha Mzalendo Kijiji cha Mawemeru , Kata ya Nyarugusu Wilaya ya Geita kwa tuhuma za kumuuwa mume wake na kumfukia katika shimo ndani nyumba yao.

Kwa mujibu wa  Kamanda wa Polisi Mkoa wa Geita, Safia Jongo taarifa ya awali inaeleza chanzo ni mgogoro wa kifamilia baina ya mke na mume ambaye kwa sasa ni marehemu.

“Baada ya mahojiano makali mwanamke huyu alikiri kwamba marehemu ni mume wake na kwamba siku hiyo ya tarehe 11 majira ya usiku mwanaume alirudi nyumbani lakini wakawa na ugomvi ambao ulisababisha kumshambulia kwa kitu chenye ncha kali na baada ya kumshambulia mwanaume huyo alifariki dunia na baada ya hapo akaamua kuchimba shimo ndani ya nyumba yao na kisha kumfukia,“ amesema  Kamanda Safia.

spot_img

Latest articles

Mchezo wa kuogelea wazidi kupaa nchini, TSA  yafichua siri

Na Winfrida  Mtoi MCHEZO wa kuogelea umezidi kushika kasi nchini  kutokana na kuongezeka idadi ya...

Dkt Nchimbi atembelea banda la Tanesco

Na Mwandishi Wetu MAKAMU wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Balozi...

Waogeleaji chipukizi 400 kutikisa Dar kesho

Na Mwandishi Wetu Zaidi ya waogeleaji 400 wenye umri wa miaka 6 hadi 12 wanatarajiwa...

Wabunge walifuata mkumbo kwenda Morocco kuishangilia Serengeti Boys lawakuta jambo

Na Mwandishi Wetu SPIKA wa Mbunge la Tanzania, Mussa Azzan Zungu ametoa siku nne za...

More like this

Mchezo wa kuogelea wazidi kupaa nchini, TSA  yafichua siri

Na Winfrida  Mtoi MCHEZO wa kuogelea umezidi kushika kasi nchini  kutokana na kuongezeka idadi ya...

Dkt Nchimbi atembelea banda la Tanesco

Na Mwandishi Wetu MAKAMU wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Balozi...

Waogeleaji chipukizi 400 kutikisa Dar kesho

Na Mwandishi Wetu Zaidi ya waogeleaji 400 wenye umri wa miaka 6 hadi 12 wanatarajiwa...