EWURA yatoa rai kuhusu vibali vya ujenzi wa Vituo vya Mafuta

Na Mwandishi Wetu

MAMLAKA ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA) imetoa rai kwa wafanyabiashara wanaokusudia kuanzisha vituo vya mafuta kuhakikisha wanapata kibali cha ujenzi kutoka EWURA kabla ya kuanza ujenzi.

Rai hiyo imetolewa leo tarehe 3 Oktoba 2025, mkoani Iringa na Meneja wa Kanda ya Kati wa EWURA, Hawa Lweno, wakati wa mkutano na wadau wa sekta ndogo za mafuta, umeme na maji.

Lweno amesema kumekuwa na mwitikio mkubwa wa wafanyabiashara kufungua vituo vya mafuta hasa maeneo ya vijijini, lakini changamoto imeibuka pale ambapo baadhi yao huanza ujenzi bila kuwa na kibali cha EWURA.

“Natoa wito kwa yeyote mwenye nia ya kuanzisha kituo cha mafuta kuhakikisha kwanza anapata kibali kutoka EWURA kabla ya kuanza ujenzi. Kukiuka sharti hili la kisheria kutasababisha mfanyabiashara husika kutozwa faini ya shilingi milioni 20,” amesema.

Kibali hicho ni muhimu kwa kuwa kinatoa nafasi kwa wataalamu wa EWURA kuhakiki na kujiridhisha kwamba ujenzi wa kituo husika unazingatia viwango na masharti ya kiafya, kiusalama na kimazingira yaliyowekwa.

Kwa upande wake, mmoja wa washiriki wa mkutano huo, David Mlyapatali, amesema kikao hicho kimekuwa na manufaa makubwa kwani kimewapa uelewa zaidi kuhusu taratibu na wajibu wao katika kuendesha biashara hizo.

spot_img

Latest articles

DCEA yateketeza kilo 504.36 za Heroin Mtwara

Na Mwandishi Wetu, Mtwara MAMLAKa ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya (DCEA) imeteketeza...

Mkurugenzi wa Rasilimali Watu Tanesco awahakikishia ushirikiano maafisa huduma kwa wateja

📌 Afunga Mkutano Mkuu wa Mwaka wa Maafisa hao 📌 Awapongeza kwa utendaji bora wenye...

Makonda  awajibu wanaoponda ziara ya Rio

Na Winfrida Mtoi WAZIRI wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Paul Makonda amesema ziara ya...

TIRDO yasajili Viwanda 25,650, Yaongeza Maabara za Kisasa Kuimarisha Sekta ya Viwanda

Na Mwandishi Wetu WIZARA ya Viwanda na Biashara kupitia Shirika la Utafiti na Maendeleo ya...

More like this

DCEA yateketeza kilo 504.36 za Heroin Mtwara

Na Mwandishi Wetu, Mtwara MAMLAKa ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya (DCEA) imeteketeza...

Mkurugenzi wa Rasilimali Watu Tanesco awahakikishia ushirikiano maafisa huduma kwa wateja

📌 Afunga Mkutano Mkuu wa Mwaka wa Maafisa hao 📌 Awapongeza kwa utendaji bora wenye...

Makonda  awajibu wanaoponda ziara ya Rio

Na Winfrida Mtoi WAZIRI wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Paul Makonda amesema ziara ya...