JBIC na JICA waahidi ushirikiano kwa ETDCO

Na Mwandishi Wetu

TAASISI ya Japan Bank for International Cooperation (JBIC) pamoja na Japan International Cooperation Agency (JICA) zimeahidi kushirikiana na Kampuni ya Ujenzi na Ukarabati wa Miundombinu ya Umeme (ETDCO) katika utekelezaji wa miradi yake ya ujenzi na ukarabati wa miundombinu ya umeme nchini Tanzania, ikiwemo uwekezaji wa kimkakati.

Wakizungumza katika vikao kazi vilivyofanyika, jijini Tokyo, Japan, viongozi kutoka JBIC na JICA wameeleza dhamira yao ya kushirikiana na ETDCO katika nyanja za uwekezaji, uhamishaji wa teknolojia na utekelezaji wa miradi ya Nishati nchini Tanzania itakayo saidia kuimarisha hali ya upatikanaji wa Nishati ya umeme.

Vikao kazi hivyo ni mwendelezo wa mafanikio ya ETDCO katika Maonesho ya Dunia (Expo 2025) yanayofanyika Osaka, Japan, ambapo Kampuni hiyo inaendelea kujitangaza kimataifa na kuimarisha mtandao wa ushirikiano kwa ajili ya kuharakisha utekelezaji wa miradi yake.

spot_img

Latest articles

Tanesco yagusa mioyo ya watoto wenye mahitaji maalum

📌Ni sehemu ya uwajibikaji wake kwa jamii 📌Yatoa misaada mbalimbali kwa vituo vitatu Dar...

 ‘Umimi’ wa viongozi unaua Jumuiya Afrika Mashariki

KATIKATI ya miaka ya 90 wakati mfumo wa vyama vingi unaota mizizi, lilitokea wazo...

Wanafunzi watatu wafariki dunia baada ya kupigwa na radi Dar

Na Mwandishi wetu WANAFUNZI watatu wa Shule ya Msingi Msongola iliyopo eneo la Msongola,...

Serikali yawataka Wakurugenzi kuongeza thamani inayopimika katika uwekezaji wa hisa chache

Na Mwandishi wetu SERIKALI imewataka wakurugenzi wa bodi za kampuni ambazo ina umiliki wa...

More like this

Tanesco yagusa mioyo ya watoto wenye mahitaji maalum

📌Ni sehemu ya uwajibikaji wake kwa jamii 📌Yatoa misaada mbalimbali kwa vituo vitatu Dar...

 ‘Umimi’ wa viongozi unaua Jumuiya Afrika Mashariki

KATIKATI ya miaka ya 90 wakati mfumo wa vyama vingi unaota mizizi, lilitokea wazo...

Wanafunzi watatu wafariki dunia baada ya kupigwa na radi Dar

Na Mwandishi wetu WANAFUNZI watatu wa Shule ya Msingi Msongola iliyopo eneo la Msongola,...