Huduma ya Maji Dar na Pwani yaimarika

Na Mwandishi Wetu

MAMLAKA ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es Salaam (DAWASA) imeendelea kuimarisha upatikanaji wa huduma ya majisafi ndani ya eneo lake la kihuduma na kuendelea kupita mtaani kujiridhisha upatikanaji wa huduma hiyo kwa Wananchi katika Mikoa ya Dar es Salaam na Pwani.

Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano DAWASA, Everlasting Lyaro ametembelea wateja katika Wilaya za Ubungo na Ilala na kujionea uimarikaji wa huduma za Maji na kusema kuwa lengo la DAWASA ni kuhakikisha kila Mwananchi anapata huduma ya Maji.

“Leo tumetembea na kuona hali ya huduma kuimarika na kwa msukumo mkubwa na sehemu nyingine huduma inaendelea kutengamaakidogo kidogo, kwa maeneo tuliyotembelea kama kwa wakazi wa Wilaya za Ubungo na Ilala katika mitaa ya Kilungule A & B, Korogwe, Ziimbili, Ulongoni A, Mongo la ndege, Kichangani, Kinyerezi, Buguruni Kisiwani, mtaa wa Ghana na Malapa hali ya huduma inaridhisha,” amesema Everlasting.

Kwa upande wake , mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa wa Kilungule A, Kaini Kyejo ameipongeza jitihada za haraka zilizofanyika na Mamlaka katika kurejesha huduma ya maji ambayo ni tegemeo la msingi katika kutekeleza majukumu mbalimbali ya kila siku majumbani.

“Wananchi wangu tayari wameanza kupata huduma ya maji na nimewatembelea lakini sio wote yanatoka kwa msukumo mkubwa lakini wamenihakikishia ni swala la muda kwa kuwa huduma inamairika,” amesema Kyejo.

Mkazi wa Mbezi Msakuzi, Alice Makamba amesema huduma ya maji kwa kipindi cha siku mbili haikuwepo lakini walipata taarifa za maboresho yanayoendelea katika Mtambo wa Ruvu juu na kwa sasa huduma imerejea na imeendelea kuimarika.

“Kwa kweli kipindi cha siku mbili huduma hatukuwa nayo lakini tulipewa taarifa kupitia mitandao ya kijamii kuwa kuna matengezo huko Ruvu Juu na huduma imerejea japo kwa msukumo haujaimarika sana ila maji tunapata,” amesema Alice.

spot_img

Latest articles

DCEA yateketeza kilo 504.36 za Heroin Mtwara

Na Mwandishi Wetu, Mtwara MAMLAKa ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya (DCEA) imeteketeza...

Mkurugenzi wa Rasilimali Watu Tanesco awahakikishia ushirikiano maafisa huduma kwa wateja

📌 Afunga Mkutano Mkuu wa Mwaka wa Maafisa hao 📌 Awapongeza kwa utendaji bora wenye...

Makonda  awajibu wanaoponda ziara ya Rio

Na Winfrida Mtoi WAZIRI wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Paul Makonda amesema ziara ya...

TIRDO yasajili Viwanda 25,650, Yaongeza Maabara za Kisasa Kuimarisha Sekta ya Viwanda

Na Mwandishi Wetu WIZARA ya Viwanda na Biashara kupitia Shirika la Utafiti na Maendeleo ya...

More like this

DCEA yateketeza kilo 504.36 za Heroin Mtwara

Na Mwandishi Wetu, Mtwara MAMLAKa ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya (DCEA) imeteketeza...

Mkurugenzi wa Rasilimali Watu Tanesco awahakikishia ushirikiano maafisa huduma kwa wateja

📌 Afunga Mkutano Mkuu wa Mwaka wa Maafisa hao 📌 Awapongeza kwa utendaji bora wenye...

Makonda  awajibu wanaoponda ziara ya Rio

Na Winfrida Mtoi WAZIRI wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Paul Makonda amesema ziara ya...