Kocha Simba aaga, atangazwa Raja Casablanca

Na Mwandishi Wetu

Aliyekuwa Kocha Mkuu wa Simba, Fadlu Davids ameaga rasmi wadau na mashabiki wa klabu hiyo na tayari ametangazwa klabu yake ya zamani ya Raja Casablanca ya nchini Morocco kukinoa kikosi hicho.

Raja Casablanca leo Septemba 22, 2025 imetoa taarifa ya mabadiliko ya benchi lake la ufundi na kumtangaza Fadlu ambaye aliwahi kutumika kama kocha msaidizi, kuwa Kocha Mkuu.

Kocha huyo hakuonekana wakati Simba ikirudi kutoka Botswana ilipokwenda mechi ya Ligi ya Mabingwa Afrika dhidi ya Gaborone United.

Fadlu aliyedumu Simba kwa kipindi cha mwaka mmoja na miezi miwili, ameaga muda mfupi baada ya kusambaa kwa tetesi kuwa kocha huyo ameachana na timu hiyo, licha ya uongozi wa Simba kushindwa kutoa  taarifa rasmi hadi sasa.

Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Fadlu ameandika walaka wa kuaga Simba unaosema: “Ni kwa moyo mzito naiaga Simba. Tangu nilipowasili, nilihisi shauku ya klabu hii kubwa na upendo wa mashabiki wake wa ajabu. Kwa pamoja tulipigana, kusherehekea, na kuimarika kupitia kila ushindi na kila changamoto.

Shukrani zangu za dhati kwa Rais Mo Dewji kwa uongozi wake wa kutia moyo, maono, na msaada wake wa kila mara.

Kwa wachezaji: endelea kupigana, endelea kuamini, na endelea kuinua beji kwa heshima. Kwa wafanyikazi na wasimamizi: asante kwa uaminifu wako na kujitolea bila kuchoka nyuma ya pazia.

Kwa mashabiki wa Simba: Wewe ndiye mapigo ya moyo wa klabu hii. Sauti zako, nyimbo zako, shauku yako isiyoyumba zitasikika katika kumbukumbu yangu. Asante kwa kukaribisha familia yangu kama yako.

Simba daima itakuwa sehemu yangu, na ninaitakia klabu mafanikio, mafanikio na vikombe mbeleni. Asanteni Sana, forever Nguvu Moja ,”

spot_img

Latest articles

Waziri wa Nishati Ndejembi azindua rasmi mita janja

Na Mwandishi Wetu WAZIRI wa Nishati, Deogratius Ndejembi amezindua rasmi mita janja (smart meter)...

RC Kunenge: Mto Ruvu ubaki kwa matumizi ya binadamu tu, tusitishe shughuli nyingine kwa muda

Na Mwandishi Wetu MKUU wa Mkoa wa Pwani, Abubakar Kunenge, ametoa wito kwa wakulima...

Tume ya Jaji Chande na mlima wenye utelezi

KAMA kuna tume ya uchunguzi iliyopata kuundwa nchini kwa jambo mahususi, ikajikuta katika uwanja...

Rais Samia: Walilenga kupindua dola

RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, amesema kuwa vurugu...

More like this

Waziri wa Nishati Ndejembi azindua rasmi mita janja

Na Mwandishi Wetu WAZIRI wa Nishati, Deogratius Ndejembi amezindua rasmi mita janja (smart meter)...

RC Kunenge: Mto Ruvu ubaki kwa matumizi ya binadamu tu, tusitishe shughuli nyingine kwa muda

Na Mwandishi Wetu MKUU wa Mkoa wa Pwani, Abubakar Kunenge, ametoa wito kwa wakulima...

Tume ya Jaji Chande na mlima wenye utelezi

KAMA kuna tume ya uchunguzi iliyopata kuundwa nchini kwa jambo mahususi, ikajikuta katika uwanja...