INEC yamteua Mpina kugombea Urais

Na Winfrida Mtoi

TUME Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC), imemteua rasmi  Luhaga Mpina kuwa Mgombea wa Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania   kupitia Chama Cha ACT Wazalendo katika uchaguzi  mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba mwaka huu.

Mpina ameteuliwa pamoja na mgombea mwenza wake, Fatma Abdulhabib  Ferej, ambapo leo Septemba 13, 2025 walifika katika Ofisi Ndogo za INEC  na  kukabidhiwa  fomu ya uteuzi na Mwenyekiti wa Tume hiyo, Jaji wa Mahakama ya Rufaa Jacobs Mwambegele.

Katika tukio hilo, Mpina aliambatana na viongozi mbalimbali waandamizi wa chama hicho pamoja na wafuasi waliokuwa wakishangilia hatua ya chama chao kufanikisha uteuzi huo.

Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Jaji wa Mahakama ya Rufaa Jacobs Mwambegele akizungumza mbele ya viongozi wa ACT Wazalendo.
Baadhi ya viongozi wa ACT Wazalendo wakiwa katika uteuzi wa mgombea Urais wa chama chao

Akizungumzia uteuzi huo, Mpina amesema hatua ya INEC kuwateua rasmi inaashiria kuwa safu yao imekamilika na watashirikiana kuhakikisha wanatumia siku za kampeni zilizobaki kufikia majimbo yote ya Tanzania.

Mpina amerejesha  fomu ikiwa ni siku mbili baada ya kushinda kesi ya kupinga kuenguliwa  kwenye mchakato wa uteuzi wa wagombea.

spot_img

Latest articles

ACT Wazalendo wakataa gari la INEC, Mpina atamba atashinda kwa asilimia 70

Na Winfrida Mtoi Chama Cha ACT Wazalendo kimegoma kupokea gari la Tume Huru ya Uchaguzi...

Mvua za vuli kunyesha kwa wastani  kuanzia  Oktoba

Na Mwandishi Wetu Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA), imetangaza kuwa msimu wa mvua...

Tembo Warriors yatinga nusu fainali CECAAF

Na Mwandishi Wetu Timu ya Taifa ya watu wenye ulemavu Tanzania 'Tembo Warriors' imefanikiwa kutinga...

Ajali yaua wanafunzi wawili wa kidato cha sita

Na Mwandishi Wetu Watu saba wamefariki dunia wakiwamo wanafunzi wawili wa kidato cha sita shule...

More like this

ACT Wazalendo wakataa gari la INEC, Mpina atamba atashinda kwa asilimia 70

Na Winfrida Mtoi Chama Cha ACT Wazalendo kimegoma kupokea gari la Tume Huru ya Uchaguzi...

Mvua za vuli kunyesha kwa wastani  kuanzia  Oktoba

Na Mwandishi Wetu Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA), imetangaza kuwa msimu wa mvua...

Tembo Warriors yatinga nusu fainali CECAAF

Na Mwandishi Wetu Timu ya Taifa ya watu wenye ulemavu Tanzania 'Tembo Warriors' imefanikiwa kutinga...