INEC yatoa wito kwa asasi za kiraia

Na Mwandishi Wetu

Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC), imezitaka taasisi na asasi za kiraia zilizopata kibali cha kutoa elimu ya mpiga kura katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2025 kutekeleza jukumu hilo kwa ufanisi na weledi.

Mkurugenzi wa Uchaguzi wa INEC, Kailima Ramadhani, ametoa wito huo leo Septemba 8, 2025, wakati wa kufungua kikao kazi kati ya Tume na taasisi pamoja na asasi hizo kilichofanyika mkoani Dodoma.

Kailima ameongeza kuwa INEC inatarajia kuona taasisi na asasi za kiraia zikitoa elimu iliyolengwa, huku zikisisitiza masuala yanayowapa wananchi, wagombea, na vyama vya siasa uelewa juu ya kushiriki katika kampeni kwa amani na utulivu, ikiwa ni pamoja na kuelewa vyema utaratibu wa kupiga kura.

“Hatutegemei kabisa mtatoa elimu itakayoichanganya jamii na kuipeleka nchi katika machafuko, kama ilivyoshuhudiwa katika baadhi ya maeneo Afrika na duniani kwa ujumla,” amesema Kailima.

Amesisitiza kuwa taasisi na asasi hizo haziruhusiwi kuwapa watu wengine, taasisi au asasi vibali walivyopewa, na kwamba vibali hivyo vinapaswa kutumiwa na walengwa pekee.

Kikao kazi hicho kimewahusisha viongozi wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi na wawakilishi wa taasisi na asasi 164 zilizopewa vibali vya kutoa elimu ya mpiga kura ambapo mada mbalimbali zimewasilishwa.

spot_img

Latest articles

Oktoba 29 siku ya giza, ifungue milango ya haki

OKTOBA 29, 2025 itabakia kuwa siku ya giza na machungu katika historia ya Jamhuri...

Fountain Gate yatoa kocha bora

Na Mwandishi Wetu Kocha wa timu ya Fountain Gate,  Mohamed Laizer amechaguliwa kuwa kocha bora...

Nyota JKT Queens aipigia hesabu Asec Mimosa

Na Winfrida Mtoi Mshambuliaji wa JKT Queens FC, Jamila Rajabu, amesema  amejipanga  kutengeneza  nafasi na...

Zungu achaguliwa kuwa Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Na Mwandishi Wetu MBUNGE mteule wa Jimbo la Ilala Mussa Azzan Zungu ameibuka mshindi...

More like this

Oktoba 29 siku ya giza, ifungue milango ya haki

OKTOBA 29, 2025 itabakia kuwa siku ya giza na machungu katika historia ya Jamhuri...

Fountain Gate yatoa kocha bora

Na Mwandishi Wetu Kocha wa timu ya Fountain Gate,  Mohamed Laizer amechaguliwa kuwa kocha bora...

Nyota JKT Queens aipigia hesabu Asec Mimosa

Na Winfrida Mtoi Mshambuliaji wa JKT Queens FC, Jamila Rajabu, amesema  amejipanga  kutengeneza  nafasi na...