Muhimbili yafafanua utaratibu wa uchangiaji figo

Na Mwandishi Wetu

Hospitali ya Taifa Muhimbili (Upanga na Mloganzila),imetoa ufafanuzi kuhusu utaratibu wa uchangiaji figo kwa wagonjwa wanaohitaji huduma ya kupandikiza viungo hivyo.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa leo Septemba 2, na Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano na Uhusiano kwa Umma wa Hospitali hiyo, Aminiel Aligaesha, huduma za upandikizaji figo zilianza kutolewa rasmi Septemba 2017 na hadi sasa wagonjwa 106 wameshanufaika.

Aligaesha amesema hospitali inazingatia Kanuni za Huduma za Figo zilizotungwa mwaka 2017 kwa kuendana na miongozo na maazimio ya Kimataifa yaliyoidhinishwa na Wizara ya Afya, ambayo yanakataza biashara ya uuzaji viungo vya binadamu.

Aidha, ameeleza kuwa ndugu wa karibu wa mgonjwa pekee ndiye anayeruhusiwa kuchangia figo na uchangiaji huo hufanyika bila malipo.

Ameongeza kuwa kuna Kamati Maalumu ya Uidhinishaji inayojumuisha wanasheria, viongozi wa dini, madaktari na maafisa ustawi wa jamii, ambayo hupitia maombi yote ya upandikizaji figo.

Kamati hiyo hukagua nyaraka za uthibitisho wa uhusiano wa damu kati ya mgonjwa na mchangiaji, ikiwamo viapo, vyeti vya kuzaliwa, picha pamoja na majibu ya vipimo vya maabara.

Hata hivyo Hospitali ya Taifa Muhimbili imesisitiza kuwa itaendelea kuhakikisha huduma ya upandikizaji figo inatolewa kwa mujibu wa kanuni zake na miongozo ya kimataifa.

spot_img

Latest articles

Waziri Gwajima aipongeza Tanesco kuandaa kongamano la wanawake la Nishati Safi ya kupikia

Na Mwandishi Wetu WAZIRI wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, Dorothy Gwajima...

Makofi, vigelegele vimemrarua Mwigulu Nchemba?

Na Jesse Kwayu KATIKA mfumo wa utawala ambao chimbuko la madaraka ya dola ni wananchi,...

Katibu Mkuu Uwekezaji afanya ziara Ofisi ya Msajili wa Hazina

Na Mwandishi Wetu KATIBU Mkuu wa Ofisi ya Rais – Uwekezaji, Dk. Fred Msemwa, leo...

DCEA yakamata Tani 9.93 za Dawa za Kulevya, Watuhumiwa 151 Watiwa Mbaroni

Na Tatu Mohamed  MAMLAKA ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya (DCEA) imekamata tani...

More like this

Waziri Gwajima aipongeza Tanesco kuandaa kongamano la wanawake la Nishati Safi ya kupikia

Na Mwandishi Wetu WAZIRI wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, Dorothy Gwajima...

Makofi, vigelegele vimemrarua Mwigulu Nchemba?

Na Jesse Kwayu KATIKA mfumo wa utawala ambao chimbuko la madaraka ya dola ni wananchi,...

Katibu Mkuu Uwekezaji afanya ziara Ofisi ya Msajili wa Hazina

Na Mwandishi Wetu KATIBU Mkuu wa Ofisi ya Rais – Uwekezaji, Dk. Fred Msemwa, leo...