Geofrey Timothy achukua fomu ya kugombea Ubunge Jimbo la Kawe

Na Mwandishi Wetu

MGOMBEA Ubunge wa Jimbo la Kawe kupitia Chama cha Mapinduzi (CCM), Geofrey Timothy, amechukua fomu ya kuwania nafasi hiyo na kuahidi kuwatumikia wananchi wa Kawe kwa ari na moyo wa kujituma.

Akizungumza leo Agosti 26, 2025 mara baada ya kuchukua fomu, Timothy ameishukuru CCM kwa imani waliyoonesha kwake kwa kumteua kupeperusha bendera ya chama hicho katika uchaguzi wa mwaka huu.

“Nashukuru viongozi wa Chama kwa kuniteua kupeperusha bendera ya chama kupitia Jimbo la Kawe. Yapo mengi tumepanga kuyafanya…nawashukuru wajumbe kwa kunipigia kura nyingi kupeperusha bendera ya chama,” amesema.

Aidha, Timothy amewataka wakazi wa Kawe kujitokeza kwa wingi katika uzinduzi wa kampeni za CCM utakaofanyika Agosti 28, 2025, akisema utakuwa ni fursa ya wananchi kusikia kwa kina mipango ya chama na kuunga mkono jitihada za Rais Samia Suluhu Hassan.

Amesema Chama hicho kimejipanga kwa mikakati thabiti ya kuendeleza utekelezaji wa Ilani kwa vitendo, ikiwemo kuboresha huduma za kijamii, kuongeza ajira kwa vijana pamoja na kukuza fursa za kiuchumi.

spot_img

Latest articles

Tanesco yagusa mioyo ya watoto wenye mahitaji maalum

📌Ni sehemu ya uwajibikaji wake kwa jamii 📌Yatoa misaada mbalimbali kwa vituo vitatu Dar...

 ‘Umimi’ wa viongozi unaua Jumuiya Afrika Mashariki

KATIKATI ya miaka ya 90 wakati mfumo wa vyama vingi unaota mizizi, lilitokea wazo...

Wanafunzi watatu wafariki dunia baada ya kupigwa na radi Dar

Na Mwandishi wetu WANAFUNZI watatu wa Shule ya Msingi Msongola iliyopo eneo la Msongola,...

Serikali yawataka Wakurugenzi kuongeza thamani inayopimika katika uwekezaji wa hisa chache

Na Mwandishi wetu SERIKALI imewataka wakurugenzi wa bodi za kampuni ambazo ina umiliki wa...

More like this

Tanesco yagusa mioyo ya watoto wenye mahitaji maalum

📌Ni sehemu ya uwajibikaji wake kwa jamii 📌Yatoa misaada mbalimbali kwa vituo vitatu Dar...

 ‘Umimi’ wa viongozi unaua Jumuiya Afrika Mashariki

KATIKATI ya miaka ya 90 wakati mfumo wa vyama vingi unaota mizizi, lilitokea wazo...

Wanafunzi watatu wafariki dunia baada ya kupigwa na radi Dar

Na Mwandishi wetu WANAFUNZI watatu wa Shule ya Msingi Msongola iliyopo eneo la Msongola,...