Geofrey Timothy achukua fomu ya kugombea Ubunge Jimbo la Kawe

Na Mwandishi Wetu

MGOMBEA Ubunge wa Jimbo la Kawe kupitia Chama cha Mapinduzi (CCM), Geofrey Timothy, amechukua fomu ya kuwania nafasi hiyo na kuahidi kuwatumikia wananchi wa Kawe kwa ari na moyo wa kujituma.

Akizungumza leo Agosti 26, 2025 mara baada ya kuchukua fomu, Timothy ameishukuru CCM kwa imani waliyoonesha kwake kwa kumteua kupeperusha bendera ya chama hicho katika uchaguzi wa mwaka huu.

“Nashukuru viongozi wa Chama kwa kuniteua kupeperusha bendera ya chama kupitia Jimbo la Kawe. Yapo mengi tumepanga kuyafanya…nawashukuru wajumbe kwa kunipigia kura nyingi kupeperusha bendera ya chama,” amesema.

Aidha, Timothy amewataka wakazi wa Kawe kujitokeza kwa wingi katika uzinduzi wa kampeni za CCM utakaofanyika Agosti 28, 2025, akisema utakuwa ni fursa ya wananchi kusikia kwa kina mipango ya chama na kuunga mkono jitihada za Rais Samia Suluhu Hassan.

Amesema Chama hicho kimejipanga kwa mikakati thabiti ya kuendeleza utekelezaji wa Ilani kwa vitendo, ikiwemo kuboresha huduma za kijamii, kuongeza ajira kwa vijana pamoja na kukuza fursa za kiuchumi.

spot_img

Latest articles

Waziri wa Nishati Ndejembi azindua rasmi mita janja

Na Mwandishi Wetu WAZIRI wa Nishati, Deogratius Ndejembi amezindua rasmi mita janja (smart meter)...

RC Kunenge: Mto Ruvu ubaki kwa matumizi ya binadamu tu, tusitishe shughuli nyingine kwa muda

Na Mwandishi Wetu MKUU wa Mkoa wa Pwani, Abubakar Kunenge, ametoa wito kwa wakulima...

Tume ya Jaji Chande na mlima wenye utelezi

KAMA kuna tume ya uchunguzi iliyopata kuundwa nchini kwa jambo mahususi, ikajikuta katika uwanja...

Rais Samia: Walilenga kupindua dola

RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, amesema kuwa vurugu...

More like this

Waziri wa Nishati Ndejembi azindua rasmi mita janja

Na Mwandishi Wetu WAZIRI wa Nishati, Deogratius Ndejembi amezindua rasmi mita janja (smart meter)...

RC Kunenge: Mto Ruvu ubaki kwa matumizi ya binadamu tu, tusitishe shughuli nyingine kwa muda

Na Mwandishi Wetu MKUU wa Mkoa wa Pwani, Abubakar Kunenge, ametoa wito kwa wakulima...

Tume ya Jaji Chande na mlima wenye utelezi

KAMA kuna tume ya uchunguzi iliyopata kuundwa nchini kwa jambo mahususi, ikajikuta katika uwanja...