Arusha kupokea ugeni mkubwa, yajiandaa kufanya utalii wa mikutano

Na Mwandishi Wetu

Kitovu cha utalii na mikutano ya kimataifa nchini, Jiji la Arusha linajiandaa kupokea wageni mbalimbali na washiriki wa kikao kazi cha wenyeviti wa Bodi na Watendaji Wakuu wa Taasisi za Umma (CEOs Forum 2025) kitakachoanza leo Agosti 23 hadi 26 katika Kituo cha Kimataifa cha Mikutano ( AICC) jijini himo.

Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Utalii Tanzania (TTB) Ephraim Mafuru amewahamasisha wageni kutumia fursa ya mkutano huo kutembelea vivutio vya kipekee vilivyopo jijini na nje ya Arusha.

“ Arusha siyo tu kitovu cha mikutano ya kimataifa bali pia ni langu Kuu la vivutio vikubwa kama Hifadhi ya Serengeti, Ngorongoro, Tarangire, Manyara, Mlima Meru na Kilimanjaro, hivyo wageni wanapaswa kushuhudia uzuri wa maeneo hayo kabla ya kuondoka, “amesema Mafuru.

Ameongeza kuwa maeneo mengine ambayo Serikali inajivunia kuyatangaza ndani ya Jiji la Arusha ni makumbusho ya elimu ya viumbe hai, makumbusho ya Manifesto, chemchem ya maji ya moto na utalii wa vyakula hususani utaalamu wa kuchoma kitoweo kwenye eneo maarufu la kwa Mromboo.

Mkutano wa CEOs Forum 2025 utahusisha mamia ya washiriki kutoka ndani na nje ya nchi, hivyo kutoa fursa ya kuonyesha urithi, vivutio na utamaduni wa Tanzania na kuimarisha diplomasia, amani na utalii.

spot_img

Latest articles

RAIS SAMIA KUZINDUA RASMI MRADI WA JNHPP AGOSTI 22, 2026

📌Waziri Ndejembi asema ni tukio la kihistoria litakaloshuhudiwa na watanzania pamoja na wageni 📌Asema...

JAJI MSHIBE ASISITIZA MAANDALIZI YA KISEKTA KATIKA KUKABILIANA NA ATHARI ZA EL NIÑO

Na Mwandishi Wetu MWENYEKITI wa Bodi ya Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA),...

Msajili wa Hazina, Fitch Ratings watathmini mageuzi ya taasisi za umma

Na Mwandishi wa OTR OFISI ya Msajili wa Hazina (OTR) Jumanne, Agosti 11, 2026, ilifanya...

More like this

RAIS SAMIA KUZINDUA RASMI MRADI WA JNHPP AGOSTI 22, 2026

📌Waziri Ndejembi asema ni tukio la kihistoria litakaloshuhudiwa na watanzania pamoja na wageni 📌Asema...

JAJI MSHIBE ASISITIZA MAANDALIZI YA KISEKTA KATIKA KUKABILIANA NA ATHARI ZA EL NIÑO

Na Mwandishi Wetu MWENYEKITI wa Bodi ya Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA),...