Jeshi la Polisi  lakabidhiwa mashine ya kuweka silaha alama

Na Mwandishi Wetu

Jeshi la Polisi nchini limekabidhiwa mashine maalumu ya kuweka alama silaha zilizopo nchini ikiwa ni hatua mbalimbali zinazochukuliwa katika kuzuia uzagaaji wa silaha ndogondogo na nyepesi ili kuepuka madhara yanayoweza kuwapata wananchi na nchi kwa ujumla.

Mashine hizo mbili zimekabidhiwa na Mwakilishi wa Taasisi ya Kikanda ya kupambana na uzagaaji wa silaha haramu na nyepesi katika Ukanda wa Maziwa Makuu na Pembe ya Afrika (RECSA), Eric Kailanga na kupokelewa na Naibu Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai Zanzibar, DCP Zuberi Chembera wakati wa ufunguzi wa mafunzo ya uwekaji alama na kutunza kumbukumbu za silaha kwa Askari Polisi jijini Dodoma.

Akizungumza baada ya kupokea mashine hizo, DCP Chembera amesema Jeshi la Polisi limeendelea kuchukua hatua mbalimbali za kuhakikisha kuwa nchi yetu inaendelea kuwa salama na kupatikana kwa mashine hizo kutasaidia kwa kiasi kikubwa juhudi hizo.

Aidha, aliwataka washiriki wa mafunzo ya uwekaji alama kuzingatia kikamilifu mafunzo watakayopata ili kuhakikisha kuwa utendaji wao unazidi kuimarika na kwenda kuwafundisha wengine ambao hawajapata fursa hiyo.

Kwa upande wake Mratibu wa Kitaifa wa Udhibiti wa Silaha ndogondogo na nyepesi nchini, Kamishna Msaidizi wa Polisi (ACP), Berthaneema Mlay amesema mashine hizo mpya walizopatiwa ni za kisasa na zitaendelea kuimarisha utendaji kazi wa kudhibiti silaha haramu nchini.

Naye Mwakilishi wa kituo cha RECSA, Eric Kayiranga amesema kituo hicho kitaendelea kushirikiana na nchi wanachama katika kuhakikisha kuwa mafunzo ya mara kwa mara yanafanyika kwa lengo la kuongeza weledi kwa vyombo na taasisi zinazosimamia sheria.

spot_img

Latest articles

Yacouba atambulishwa Mbeya City

Na Mwandishi Wetu NYOTA wa zamani wa Yanga, raia wa Burkina Faso, Yacouba Songne, ametambulishwa ...

Waziri Ndejembi: Tanzania ina fursa kubwa ya kuendeleza nishati ya Jotoardhi

Na Mwandishi Wetu WAZIRI wa Nishati, Deogratius Ndejembi, amesema kutokana na uwepo wa vyanzo...

‘Guardians of the Peak’ kuinua utangazaji utalii wa Kilimanjaro kupitia filamu

Na Mwandishi Wetu MRADI wa Guardians of the Peak, unaoingia msimu wake wa pili,...

Serikali yazindua Jukwaa la Vijana, yataja vijana kuwa mhimili Mkuu wa Maendeleo ya Taifa

Na Tatu Mohamed SERIKALI imezindua rasmi jukwaa la kitaifa la vijana lijulikanalo kama ‘Vijana...

More like this

Yacouba atambulishwa Mbeya City

Na Mwandishi Wetu NYOTA wa zamani wa Yanga, raia wa Burkina Faso, Yacouba Songne, ametambulishwa ...

Waziri Ndejembi: Tanzania ina fursa kubwa ya kuendeleza nishati ya Jotoardhi

Na Mwandishi Wetu WAZIRI wa Nishati, Deogratius Ndejembi, amesema kutokana na uwepo wa vyanzo...

‘Guardians of the Peak’ kuinua utangazaji utalii wa Kilimanjaro kupitia filamu

Na Mwandishi Wetu MRADI wa Guardians of the Peak, unaoingia msimu wake wa pili,...