Jeshi la Polisi  lakabidhiwa mashine ya kuweka silaha alama

Na Mwandishi Wetu

Jeshi la Polisi nchini limekabidhiwa mashine maalumu ya kuweka alama silaha zilizopo nchini ikiwa ni hatua mbalimbali zinazochukuliwa katika kuzuia uzagaaji wa silaha ndogondogo na nyepesi ili kuepuka madhara yanayoweza kuwapata wananchi na nchi kwa ujumla.

Mashine hizo mbili zimekabidhiwa na Mwakilishi wa Taasisi ya Kikanda ya kupambana na uzagaaji wa silaha haramu na nyepesi katika Ukanda wa Maziwa Makuu na Pembe ya Afrika (RECSA), Eric Kailanga na kupokelewa na Naibu Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai Zanzibar, DCP Zuberi Chembera wakati wa ufunguzi wa mafunzo ya uwekaji alama na kutunza kumbukumbu za silaha kwa Askari Polisi jijini Dodoma.

Akizungumza baada ya kupokea mashine hizo, DCP Chembera amesema Jeshi la Polisi limeendelea kuchukua hatua mbalimbali za kuhakikisha kuwa nchi yetu inaendelea kuwa salama na kupatikana kwa mashine hizo kutasaidia kwa kiasi kikubwa juhudi hizo.

Aidha, aliwataka washiriki wa mafunzo ya uwekaji alama kuzingatia kikamilifu mafunzo watakayopata ili kuhakikisha kuwa utendaji wao unazidi kuimarika na kwenda kuwafundisha wengine ambao hawajapata fursa hiyo.

Kwa upande wake Mratibu wa Kitaifa wa Udhibiti wa Silaha ndogondogo na nyepesi nchini, Kamishna Msaidizi wa Polisi (ACP), Berthaneema Mlay amesema mashine hizo mpya walizopatiwa ni za kisasa na zitaendelea kuimarisha utendaji kazi wa kudhibiti silaha haramu nchini.

Naye Mwakilishi wa kituo cha RECSA, Eric Kayiranga amesema kituo hicho kitaendelea kushirikiana na nchi wanachama katika kuhakikisha kuwa mafunzo ya mara kwa mara yanafanyika kwa lengo la kuongeza weledi kwa vyombo na taasisi zinazosimamia sheria.

spot_img

Latest articles

Mchezo wa kuogelea wazidi kupaa nchini, TSA  yafichua siri

Na Winfrida  Mtoi MCHEZO wa kuogelea umezidi kushika kasi nchini  kutokana na kuongezeka idadi ya...

Dkt Nchimbi atembelea banda la Tanesco

Na Mwandishi Wetu MAKAMU wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Balozi...

Waogeleaji chipukizi 400 kutikisa Dar kesho

Na Mwandishi Wetu Zaidi ya waogeleaji 400 wenye umri wa miaka 6 hadi 12 wanatarajiwa...

Wabunge walifuata mkumbo kwenda Morocco kuishangilia Serengeti Boys lawakuta jambo

Na Mwandishi Wetu SPIKA wa Mbunge la Tanzania, Mussa Azzan Zungu ametoa siku nne za...

More like this

Mchezo wa kuogelea wazidi kupaa nchini, TSA  yafichua siri

Na Winfrida  Mtoi MCHEZO wa kuogelea umezidi kushika kasi nchini  kutokana na kuongezeka idadi ya...

Dkt Nchimbi atembelea banda la Tanesco

Na Mwandishi Wetu MAKAMU wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Balozi...

Waogeleaji chipukizi 400 kutikisa Dar kesho

Na Mwandishi Wetu Zaidi ya waogeleaji 400 wenye umri wa miaka 6 hadi 12 wanatarajiwa...