Yanga yafuta taarifa ya ufafanuzi wa milioni 100, Chadema yawajia juu viongozi wa klabu

Na Mwandishi Wetu

Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimewataka viongozi wa klabu ya  Yanga, kutathmini uhalali wao wa kuongoza klabu hiyo kwa kitendo cha kukichangia Chama Cha Mapinduzi (CCM)  sh 100 milioni.

Taarifa ya Chadema iliyotolewa leo tarehe 15 Agosti 2025, na Mkurugenzi wa Mawasiliano wa  Chadema, Brenda Rupia.

Katika taarifa hiyo Rupia ameeleza kuwa kitendo cha Yanga kuichangia CCM ni dharau kwa wanachama na mashabiki wenye itikadi za vyama mbalimbali za siasa.

Rupia ameeleza kuwa taarifa ya yanga ya kudai kuwa mchango huo ulitoka kwa GSM haikuwa ya kweli kwa kuwa taarifa za awali zilidai kuwa GSM, amechangia sh.10 Bilioni, huku Yanga ikichangia sh.100 milioni.

Katika hatua nyingine Yanga imeondoa katika mitandao yake ya kijamii  taarifa ya ufafanuzi waliyoandika kwa Umma jana juu ya mchango huo, pamoja na kuwaomba radhi mashabiki waliyoitoa jana Agosti 14,2025.

spot_img

Latest articles

Muswada wa Sheria ya Uwekezaji wa Umma kukamilika 2026/27

Na Mwandishi wetu KATIKA kuendelea kuimarisha uwekezaji wa umma, Serikali imepanga kukamilisha Muswada wa...

Kocha Bilo afariki dunia

Na Mwandishi Wetu MMILIKI wa Kituo cha Soka cha Bilo Jijini Mwanza, Kocha Athuman Bilal...

Tukatae kunyweshwa sumu hii

“Kama taifa letu lilipata kuwa na bahati ni kuwa na Rais aliyechukia rushwa kama...

Chipukizi wa kuogelea kushindana ‘ East Africa Development Swimming Gala’

Na Mwandishi Wetu ZAIDI ya waogeleji 600 wanatarajiwa kushiriki katika mashindano ya kuogelea ya chipukizi...

More like this

Muswada wa Sheria ya Uwekezaji wa Umma kukamilika 2026/27

Na Mwandishi wetu KATIKA kuendelea kuimarisha uwekezaji wa umma, Serikali imepanga kukamilisha Muswada wa...

Kocha Bilo afariki dunia

Na Mwandishi Wetu MMILIKI wa Kituo cha Soka cha Bilo Jijini Mwanza, Kocha Athuman Bilal...

Tukatae kunyweshwa sumu hii

“Kama taifa letu lilipata kuwa na bahati ni kuwa na Rais aliyechukia rushwa kama...