Wananchi Manispaa ya Kigoma Ujiji waanza kunufaika na Mradi wa Tactic

Na Mwandishi Wetu, Kigoma

WANANCHI katika Manispaa ya Kigoma Ujiji wameanza kunufaika na mradi wa TACTIC unaotekelezwa chini ya Wakala ya Barabara za Vijijini na Mijini (TARURA) kwa mkopo nafuu kutoka Benki ya Dunia.

Akielezea mradi huo unavyotekelezwa katika Manispaa ya Kigoma Ujiji , Mkurugenzi Mtendaji wa Manispaa hiyo, Kisena Mabuba amesema kuwa mradi huo umejikita katika uboreshaji wa miundombinu ambapo kwa Manispaa hiyo kazi zinazofanyika ni pamoja na ujenzi wa mitaro ya maji, ujenzi wa daraja, masoko na barabara.

Aidha, ameongeza kuwa miundombinu hiyo inayojengwa inalenga kukuza uchumi wa wananchi na kuondoa kero za usafiri na usafirishaji huku akibainisha kuwa kipindi cha masika wananchi walikua wanapata shida kwani maji yaliingia katika makazi yao lakini kupitia mradi wa TACTIC tayari mitaro imejengwa na maji yanaelekezwa moja kwa moja ziwani.

“Kupitia mradi huu, tutapata barabara za kiwango cha lami zenye urefu wa kilomita 9.5 ambazo zitaunganisha Kata sita za Manispaa yetu, uwepo wa taa za barabarani pia utapendezesha Mji wetu,” amesema .

Kwa upande wake Mhandisi Julius Samwel ambaye ni mratibu wa mradi wa TACTIC ngazi ya Manispaa amesema kuwa miradi yote imeanza na utekelezaji wake upo katika hatua mbalimbali.

Wakiongea kuhusu miradi hiyo wananchi wa Manispaa ya Kigoma Ujiji wameonesha furaha yao juu ya utatuzi wa kero ya muda mrefu.

Mariam Athumani ambaye ni Mkazi wa Kigoma Ujiji amesema kuwa kabla ya ujenzi wa mifereji ,maji yaliingia katika makazi na kusababisha kero na uharibifu wa mali lakini kwa sasa yameelekezwa moja kwa moja ziwani.

Akiongea kuhusu ujenzi wa Soko la Mwanga, Hussein Hamis ambaye ni mkazi wa Manispaa ya Kigoma amesema kuwa kukamilika kwa soko hilo kutachochea uchumi wa Mkoa kwani watapata wageni mbalimbali kutoka nchi za jirani zikiwemo Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo na Burundi ambao watafika kufanya biashara.

Kuhusu ujenzi wa Soko la samaki Katonga, wafanyabiashara wameipongeza Serikali kuleta mradi huo utakaowawezesha kufanya biashara kwa njia za kisasa na kukuza uchumi .

spot_img

Latest articles

Ofisi ya Msajili wa Hazina yatoa wito wa utawala bora kuimarisha uwekezaji wa umma

Na Mwandishi Wetu OFISI ya Msajili wa Hazina (OMH) imesisitiza kuwa mustakabali wa mafanikio...

TTB yamkaribisha bingwa wa Masumbwi duniani Terence kwa ziara ya utalii

Na Mwandishi Wetu MKURUGENZI wa Bodi ya Utalii Tanzania (TTB), Ephraim Mafuru, amemkaribisha nchini...

DAWASA yasisitiza matumizi ya bidhaa za ndani kuimarisha huduma ya maji

Na Mwandishi Wetu MAMLAKA ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es Salaam (DAWASA)...

DCEA yateketeza kilo 504.36 za Heroin Mtwara

Na Mwandishi Wetu, Mtwara MAMLAKa ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya (DCEA) imeteketeza...

More like this

Ofisi ya Msajili wa Hazina yatoa wito wa utawala bora kuimarisha uwekezaji wa umma

Na Mwandishi Wetu OFISI ya Msajili wa Hazina (OMH) imesisitiza kuwa mustakabali wa mafanikio...

TTB yamkaribisha bingwa wa Masumbwi duniani Terence kwa ziara ya utalii

Na Mwandishi Wetu MKURUGENZI wa Bodi ya Utalii Tanzania (TTB), Ephraim Mafuru, amemkaribisha nchini...

DAWASA yasisitiza matumizi ya bidhaa za ndani kuimarisha huduma ya maji

Na Mwandishi Wetu MAMLAKA ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es Salaam (DAWASA)...