Taifa Stars yaandika historia CHAN, yatinga robo fainali kibabe

Na Mwandishi Wetu

Timu ya Taifa ya Tanzania ‘Taifa Stars’ imeandika historia kwa mara kwanza kwa kutinga robo fainali ya michuano ya CHAN ikiichapa Madagascar mabao 2-1 katika mchezo uliopigwa leo Agosti 9, 2025 Uwanja wa Benjamin Mkapa, Dar es Salaam.

Stars iliyopo kundi B imefikisha pointi tisa, huku ikiwa imebakiwa na mechi moja dhidi ya Afrika ya Kati ambayo inaburuza mkia katika kundi hilo.

Taifa Stars imekuwa timu ya kwanza kutinga robo fainali katika michuano hiyo ikiwa haijapoteza mechi hata moja katika tatu ilizocheza.

Ilianza mechi ya ufunguzi ya michuano hiyo kwa kuitandika Burkina Faso mabao 2-0, ikaichapa Mauritania bao 1-0 na leo kuikung’uta Madagascar 2-1, mechi zote zikipigwa dimba la Mkapa.

Ukiangalia msimamo ulivyo katika kundi B, Burkina Faso pekew ndiyo ina uwezo wa kufikisha kufikia alama tisa kutokana na kucheza mechi mbili na kupata pointi tatu, imebakiza michezo miwili.

Nafasi ya pili ipo Mauritania na pointi nne ikicheza mechi tatu, namba tatu ni Madagascar yenye alama moja na imecheza michezo miwili, mwisho yupo Afrika ya Kati aliyecheza mechi tatu bila kupata pointi yoyote.

spot_img

Latest articles

Kamati ya kudumu ya Binge Nishati na Madini yaridhishwa na maendeleo ya Kiwanda cha nguzo za zege

📌Ni mradi wa kihistoria kutekelezwa chini ya Serikali ya awamu ya Sita 📌 Yaipongeza...

Waziri Ulega, RC Chalamila pekueni mafaili wizarani

KWA nyakati tofauti viongozi wawili wamezungumzia jiji la Dar es Salaam kuhusu msongamano wa...

Rais Samia amuasili mtoto mchanga aliyetelekezwa Nzega

Na Mwandishi Wetu RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, ,Samia Suluhu Hassan, amemuasili mtoto...

Beki Yanga afanyiwa upasuaji Afrika Kusini

Na Mwandishi Wetu NAHODHA msaidizi wa timu ya Yanga na mchezaji wa timu ya Taifa...

More like this

Kamati ya kudumu ya Binge Nishati na Madini yaridhishwa na maendeleo ya Kiwanda cha nguzo za zege

📌Ni mradi wa kihistoria kutekelezwa chini ya Serikali ya awamu ya Sita 📌 Yaipongeza...

Waziri Ulega, RC Chalamila pekueni mafaili wizarani

KWA nyakati tofauti viongozi wawili wamezungumzia jiji la Dar es Salaam kuhusu msongamano wa...

Rais Samia amuasili mtoto mchanga aliyetelekezwa Nzega

Na Mwandishi Wetu RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, ,Samia Suluhu Hassan, amemuasili mtoto...