Salum Mwalimu mgombea urais Chaumma, Devota Minja mgombea mwenza

Na Mwandishi Wetu

CHAMA cha Ukombozi wa Umma (Chaumma), kimemtangaza Salum Mwalimu kuwa mgombea wa Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwenye uchaguzi mkuu utakaofanyika Oktoba 29, 2025.

Uamuzi huo umetangazwa leo Agosti 7, 2025 na Naibu Katibu Mkuu wa Chaumma, Benson Kigaila kwenye Mkutano Mkuu wa chama hicho uliofanyika ukumbi wa Mlimani City, Dar es Salaam.

Amesema jina la Mwalimu lilipendekezwa na Halmashauri Kuu ya Taifa ya chama hicho yenye jukumu la kuleta mapendekezo ya jina la mgombea urais Tanzania na Zanzibar katika kikao kilichofanyika jana.

Baada ya kutangazwa mgombea urais chama hicho, Mwalimu amemteua Devotha Minja kuwa mgombea mwenza katika uchaguzi mkuu.

Salum Mwalimu na Devotha ni wanasiasa waliojiunga na chama hicho mwaka huu wakitokea Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) ambako waliwahi kuwa katika nafasi mbalimbali za uongozi.

Katika hatua nyingine Chaumma kimeidhinisha rasmi ilani yake ya uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba 29, 2025.

spot_img

Latest articles

DAWASA yafafanua sababu ya ukosefu wa maji maeneo ya Kibaha hadi Kisarawe

Na Mwandishi Wetu MAMLAKA ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es Salaam (DAWASA)...

Tanesco yatambuliwa kama sekta wezeshi na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM)

📍Yapokea cheti cha pongezi kwa mchango wake katika kuendeleza elimu jumuishi 📍Utambuzi watolewa katika hafla...

DAWASA yaanza kufunga Pampu zitakazoimarisha huduma ya Maji

Na Mwandishi Wetu MAMLAKA ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es Salaam (DAWASA),...

TPDC Yahimiza Wananchi Kulinda Miundombinu ya Bomba la Gesi Asilia

Na Mwandishi Wetu SHIRIKA la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC) limeendelea kuwashirikisha wananchi...

More like this

DAWASA yafafanua sababu ya ukosefu wa maji maeneo ya Kibaha hadi Kisarawe

Na Mwandishi Wetu MAMLAKA ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es Salaam (DAWASA)...

Tanesco yatambuliwa kama sekta wezeshi na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM)

📍Yapokea cheti cha pongezi kwa mchango wake katika kuendeleza elimu jumuishi 📍Utambuzi watolewa katika hafla...

DAWASA yaanza kufunga Pampu zitakazoimarisha huduma ya Maji

Na Mwandishi Wetu MAMLAKA ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es Salaam (DAWASA),...