Salum Mwalimu mgombea urais Chaumma, Devota Minja mgombea mwenza

Na Mwandishi Wetu

CHAMA cha Ukombozi wa Umma (Chaumma), kimemtangaza Salum Mwalimu kuwa mgombea wa Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwenye uchaguzi mkuu utakaofanyika Oktoba 29, 2025.

Uamuzi huo umetangazwa leo Agosti 7, 2025 na Naibu Katibu Mkuu wa Chaumma, Benson Kigaila kwenye Mkutano Mkuu wa chama hicho uliofanyika ukumbi wa Mlimani City, Dar es Salaam.

Amesema jina la Mwalimu lilipendekezwa na Halmashauri Kuu ya Taifa ya chama hicho yenye jukumu la kuleta mapendekezo ya jina la mgombea urais Tanzania na Zanzibar katika kikao kilichofanyika jana.

Baada ya kutangazwa mgombea urais chama hicho, Mwalimu amemteua Devotha Minja kuwa mgombea mwenza katika uchaguzi mkuu.

Salum Mwalimu na Devotha ni wanasiasa waliojiunga na chama hicho mwaka huu wakitokea Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) ambako waliwahi kuwa katika nafasi mbalimbali za uongozi.

Katika hatua nyingine Chaumma kimeidhinisha rasmi ilani yake ya uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba 29, 2025.

spot_img

Latest articles

Jeuri ya ushindi CAFCL Simba waanza ‘kuchonga’

Na Winfrida Mtoi Ushindi wa mabao 3-0 ugenini dhidi ya Nsingizini Hotspurs katika mchezo wa Ligi ya...

Viongozi wa dini wahimiza Watanzania kupiga kura, amani

Na Mwandishi Wetu, Mwanza VIONGOZI wa dini mbalimbali mkoani Mwanza, wametoa wito kwa Watanzania kujitokeza...

Chalamila amkabidhi mjane Alice Haule Hati ya Nyumba

Na Tatu Mohamed MKUU wa Mkoa wa Dar es Salaam, Albert Chalamila, amemkabidhi hati ya...

Rasmi Kocha Yanga afungashiwa virago usiku

Na Mwandishi Wetu Uongozi wa Klabu ya Yanga umevunja mkataba na Kocha Mkuu, Romain Folz. ...

More like this

Jeuri ya ushindi CAFCL Simba waanza ‘kuchonga’

Na Winfrida Mtoi Ushindi wa mabao 3-0 ugenini dhidi ya Nsingizini Hotspurs katika mchezo wa Ligi ya...

Viongozi wa dini wahimiza Watanzania kupiga kura, amani

Na Mwandishi Wetu, Mwanza VIONGOZI wa dini mbalimbali mkoani Mwanza, wametoa wito kwa Watanzania kujitokeza...

Chalamila amkabidhi mjane Alice Haule Hati ya Nyumba

Na Tatu Mohamed MKUU wa Mkoa wa Dar es Salaam, Albert Chalamila, amemkabidhi hati ya...