Mfanyabiashara ahukumiwa jela maisha kwa kumbaka mtoto wa miaka minne

Na Mwandishi Wetu

Mahakama ya Wilaya ya Mbozi imemtia hatiani na kumhukumu kifungocha maisha gerezani, mfanyabiashara Athuman Mtibwa (35) na kulipa kiasi cha fidia milioni moja kwa mwathirika kwa kosa la kubaka mtoto wa miaka minne.

Kwa mujibu wa taarifa iliyokwa kwenye mtandao wa kijamii  @polisi.tanzania  Mtimbwa alikamatwa Oktoba 21, 2024 maeneo ya kiwandani Mlowo, Wilaya ya Mbozi, ilielezwa mahakamani hapo kuwa, mshtakiwa alitekeleza tukio hilo la ubakaji kwa kumvizia mwanafunzi huyo wa darasa la awali akiwa anatoka shule na kumvuta kwa nguvu kisha kumuingiza katika kibanda chake cha biashara na kumbaka.

Akitoa hukumu hiyo Julai 29, 2025 kesi namba 32392 ya mwaka 2024, Hakimu mkazi wa Wilaya ya Mbozi,Nemes Chami alisema Mahakama imejiridhisha pasipo na shaka ushahidi uliotolewa na upande wa Jamhuri na kumtia hatiani mtuhumiwa huyo.

“Mshtakiwa amehukumiwa kifungo pamoja na fidia hiyo ili iwe fundisho kwa watu wengine wanaojihusisha na vitendo vya ukatili wa kijinsia dhidi ya watoto,”

spot_img

Latest articles

DCEA yakamata Lita 66,048 za kemikali bashirifu

NA MWANDISHI WETU MAMLAKA ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya ((DCEA), imefanikiwa kukamata...

Chevron yaonesha nia ya kuwekeza Tanzania katika sekta ndogo ya Mafuta na Gesi Asilia

Na Mwandishi Wetu KAMPUNI kubwa ya nishati kutoka Marekani, Chevron Corporation imeeleza utayari wake wa...

Jumba la maajabu laiponza Yanga,  yapigwa faini  milioni 30,  Meneja  matatani

Na Mwandishi Wetu KLABU ya Yanga imetozwa faini ya Sh 30 milioni  kwa kosa la...

Waziri Ndejembi atoa maelekezo mazito utekelezaji wa mradi Malagarasi MW 49.6 KIGOMA

📌Hajaridhishwa na kasi ya utekelezaji wa mkandarasi kwenye mradi 📌Aagiza ukaguzi maalum wa matumizi ya...

More like this

DCEA yakamata Lita 66,048 za kemikali bashirifu

NA MWANDISHI WETU MAMLAKA ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya ((DCEA), imefanikiwa kukamata...

Chevron yaonesha nia ya kuwekeza Tanzania katika sekta ndogo ya Mafuta na Gesi Asilia

Na Mwandishi Wetu KAMPUNI kubwa ya nishati kutoka Marekani, Chevron Corporation imeeleza utayari wake wa...

Jumba la maajabu laiponza Yanga,  yapigwa faini  milioni 30,  Meneja  matatani

Na Mwandishi Wetu KLABU ya Yanga imetozwa faini ya Sh 30 milioni  kwa kosa la...