Mfanyabiashara ahukumiwa jela maisha kwa kumbaka mtoto wa miaka minne

Na Mwandishi Wetu

Mahakama ya Wilaya ya Mbozi imemtia hatiani na kumhukumu kifungocha maisha gerezani, mfanyabiashara Athuman Mtibwa (35) na kulipa kiasi cha fidia milioni moja kwa mwathirika kwa kosa la kubaka mtoto wa miaka minne.

Kwa mujibu wa taarifa iliyokwa kwenye mtandao wa kijamii  @polisi.tanzania  Mtimbwa alikamatwa Oktoba 21, 2024 maeneo ya kiwandani Mlowo, Wilaya ya Mbozi, ilielezwa mahakamani hapo kuwa, mshtakiwa alitekeleza tukio hilo la ubakaji kwa kumvizia mwanafunzi huyo wa darasa la awali akiwa anatoka shule na kumvuta kwa nguvu kisha kumuingiza katika kibanda chake cha biashara na kumbaka.

Akitoa hukumu hiyo Julai 29, 2025 kesi namba 32392 ya mwaka 2024, Hakimu mkazi wa Wilaya ya Mbozi,Nemes Chami alisema Mahakama imejiridhisha pasipo na shaka ushahidi uliotolewa na upande wa Jamhuri na kumtia hatiani mtuhumiwa huyo.

“Mshtakiwa amehukumiwa kifungo pamoja na fidia hiyo ili iwe fundisho kwa watu wengine wanaojihusisha na vitendo vya ukatili wa kijinsia dhidi ya watoto,”

spot_img

Latest articles

Serikali kuendelea kuwawezesha vijana kijamii, kiuchumi

Na Tatu Mohamed WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Rais – Maendeleo ya Vijana, Joel...

Kids Holiday Festival yawavuta mamia ya watoto, CRDB yatumia jukwaa kujenga uelewa wa fedha

Na Mwandishi Wetu BURUDANI na michezo mbalimbali vilitawala Tamasha la Kids Holiday Festival lililowakusanya...

Mambo: Demokrasia haijengwi kwa mashinikizo, vitisho

Na Mwandishi Wetu ALIYEKUWA Mgombea wa Bavicha Taifa, Masoud Mambo amesema kuwa demokrasia ya...

Serikali yaahidi kuimarisha uwezeshaji wa Makundi Maalum kupitia ajenda ya Maendeleo Jumuishi

Na Tatu Mohamed WAZIRI wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, Dkt....

More like this

Serikali kuendelea kuwawezesha vijana kijamii, kiuchumi

Na Tatu Mohamed WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Rais – Maendeleo ya Vijana, Joel...

Kids Holiday Festival yawavuta mamia ya watoto, CRDB yatumia jukwaa kujenga uelewa wa fedha

Na Mwandishi Wetu BURUDANI na michezo mbalimbali vilitawala Tamasha la Kids Holiday Festival lililowakusanya...

Mambo: Demokrasia haijengwi kwa mashinikizo, vitisho

Na Mwandishi Wetu ALIYEKUWA Mgombea wa Bavicha Taifa, Masoud Mambo amesema kuwa demokrasia ya...