TIRDO yawahimiza Watanzania kutumia mkaa mbadala

Na Tatu Mohamed, Dodoma

SHIRIKA la Utafiti wa Maendeleo ya Viwanda Tanzania (TIRDO) limewahimiza Watanzania kuachana na matumizi ya kuni na mkaa wa miti na badala yake kutumia mkaa unaotengenezwa kutokana na mabaki ya mazao mashambani, ili kulinda mazingira na kukuza matumizi ya nishati safi ya kupikia.

Wito huo umetolewa jijini Dodoma na Mhandisi Paul Josephat Kimati, kutoka TIRDO, wakati akizungumza na waandishi wa habari katika Maonesho ya Wakulima na Wafugaji kitaifa(Nanenane) yanayoendelea mkoani humo.

Mhandisi Kimati amesema kuwa TIRDO imefanya utafiti wa kina kufuatia Agenda ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, kuhusu nishati safi ya kupikia, na kwamba mkaa unaotokana na mabaki ya mazao ni njia mojawapo ya kutimiza dhamira hiyo.

“Tumetafiti kwenye mabaki ya mazao mashambani, ikiwemo vifuu vya nazi, vifuu vya chikichi, maranda ya mbao, mabaki ya mpunga na magunzi ya mahindi. Vyote hivi vikitumika vizuri vinaweza kutoa mkaa wa ubora na gharama nafuu,” amesema Mhandisi Kimati.

Aidha, amesema mkaa huo si tu kwamba ni rafiki kwa mazingira, bali pia ni nafuu na unaweza kuzalishwa kwa kutumia teknolojia rahisi inayopatikana hapa nchini.

Ameongeza kuwa TIRDO ipo tayari kutoa mafunzo kwa wafanyabiashara na wadau mbalimbali wanaopenda kujifunza kuhusu teknolojia hiyo, na kuwakaribisha katika ofisi zao kwa ajili ya kujifunza kwa vitendo.

“Tunawaalika wafanyabiashara, wakulima na wadau wengine kutembelea banda letu hapa Nanenane ili wajifunze na kuona kwa macho yao teknolojia tunazotumia katika kuzalisha mkaa huu mbadala,” amesema.

Hatua hii ya TIRDO inakuja wakati ambapo nchi inaendelea kuhamasisha matumizi ya nishati mbadala, kwa lengo la kupunguza uharibifu wa mazingira unaotokana na ukataji miti hovyo kwa ajili ya kuni na mkaa wa mawe.

spot_img

Latest articles

Jeuri ya ushindi CAFCL Simba waanza ‘kuchonga’

Na Winfrida Mtoi Ushindi wa mabao 3-0 ugenini dhidi ya Nsingizini Hotspurs katika mchezo wa Ligi ya...

Viongozi wa dini wahimiza Watanzania kupiga kura, amani

Na Mwandishi Wetu, Mwanza VIONGOZI wa dini mbalimbali mkoani Mwanza, wametoa wito kwa Watanzania kujitokeza...

Chalamila amkabidhi mjane Alice Haule Hati ya Nyumba

Na Tatu Mohamed MKUU wa Mkoa wa Dar es Salaam, Albert Chalamila, amemkabidhi hati ya...

Rasmi Kocha Yanga afungashiwa virago usiku

Na Mwandishi Wetu Uongozi wa Klabu ya Yanga umevunja mkataba na Kocha Mkuu, Romain Folz. ...

More like this

Jeuri ya ushindi CAFCL Simba waanza ‘kuchonga’

Na Winfrida Mtoi Ushindi wa mabao 3-0 ugenini dhidi ya Nsingizini Hotspurs katika mchezo wa Ligi ya...

Viongozi wa dini wahimiza Watanzania kupiga kura, amani

Na Mwandishi Wetu, Mwanza VIONGOZI wa dini mbalimbali mkoani Mwanza, wametoa wito kwa Watanzania kujitokeza...

Chalamila amkabidhi mjane Alice Haule Hati ya Nyumba

Na Tatu Mohamed MKUU wa Mkoa wa Dar es Salaam, Albert Chalamila, amemkabidhi hati ya...