DED Mkalama: Wizara ya Nishati endeleeni kusimamia ufanisi wa miradi ya nishati

Na Mwandishi Wetu

MKURUGENZI wa Wilaya ya Mkalama, Mkoani Singida, Asia Juma Messos ametoa wito kwa Wizara ya Nishati kuendelea kusimamia vyema Taasisi zake ili ziendelee kutekeleza miradi ya Sekta ya Nishati kwa ufanisi na hivyo kuleta maendeleo kwa Wananchi.

Messos amesema hayo Agosti 6, 2025 wakati alipoitembelea Banda la Wizara ya Nishati na Taasisi zake katika Maonesho ya Kimataifa ya Kilimo ( Nanenane) Jijini Dodoma.

Ameeleza kuwa Serikali imekuwa ikitoa fedha nyingi kutekeleza miradi mbalimbali ya maendeleo kwa Wananchi ikiwemo miradi ya umeme na Gesi Asilia hivyo Wizara iendelee kuzisimamia Taasisi zake, ziweze kutekeleza miradi hiyo kwa ufanisi.

Mkurugenzi wa Wilaya ya Mkalama pia ametembelea Mabanda ya Taasisi za Wizara ambazo ni TANESCO, REA, EWURA, PURA, TPDC, PBPA na TGDC ili kuona shughuli mbalimbali zinazofanywa katika Maonesho hayo.

Katika ziaza hiyo Messos ameambatana na Katibu Tawala Wilaya ya Mpwapwa, Michael Maganga, Katibu Tawala Wilaya ya Dodoma, Sakina Mbugi na Mkurugenzi Msaidizi wa Utawala kutoka Wizara ya Kilimo, Eliasifu Mlay.

spot_img

Latest articles

DAWASA yafafanua sababu ya ukosefu wa maji maeneo ya Kibaha hadi Kisarawe

Na Mwandishi Wetu MAMLAKA ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es Salaam (DAWASA)...

Tanesco yatambuliwa kama sekta wezeshi na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM)

📍Yapokea cheti cha pongezi kwa mchango wake katika kuendeleza elimu jumuishi 📍Utambuzi watolewa katika hafla...

DAWASA yaanza kufunga Pampu zitakazoimarisha huduma ya Maji

Na Mwandishi Wetu MAMLAKA ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es Salaam (DAWASA),...

TPDC Yahimiza Wananchi Kulinda Miundombinu ya Bomba la Gesi Asilia

Na Mwandishi Wetu SHIRIKA la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC) limeendelea kuwashirikisha wananchi...

More like this

DAWASA yafafanua sababu ya ukosefu wa maji maeneo ya Kibaha hadi Kisarawe

Na Mwandishi Wetu MAMLAKA ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es Salaam (DAWASA)...

Tanesco yatambuliwa kama sekta wezeshi na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM)

📍Yapokea cheti cha pongezi kwa mchango wake katika kuendeleza elimu jumuishi 📍Utambuzi watolewa katika hafla...

DAWASA yaanza kufunga Pampu zitakazoimarisha huduma ya Maji

Na Mwandishi Wetu MAMLAKA ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es Salaam (DAWASA),...