DC Kondoa avutiwa na hamasa ya kilimo cha mkonge Dodoma

Na Mwandishi Wetu

MKUU wa Wilaya ya Kondoa, Fatma Nyangassa, amepongeza juhudi zinazofanywa na Bodi ya Mkonge Tanzania (TSB) katika kuhamasisha kilimo cha mkonge, ambazo zimewezesha kupatikana kwa zaidi ya wakulima 15 wenye jumla ya ekari 240 ndani ya muda mfupi.

Akizungumza leo Jumatano mara baada ya kutembelea banda la TSB katika Maonesho ya Kimataifa ya Kilimo, Uvuvi na Mifugo yanayoendelea katika Viwanja vya Nzuguni, Fatma amesema ameridhishwa na hatua hiyo, huku akionesha nia ya kuona Mkoa wa Dodoma, hususan Wilaya ya Kondoa, inakuwa kinara wa uzalishaji wa zao hilo.

“Nimefurahishwa sana na kazi nzuri mnayofanya, na matarajio yangu ni kuona Wilaya ya Kondoa inaongoza kwa uzalishaji wa mkonge,” amesema Fatma.

Kwa upande wake, Mkuu wa Sehemu ya Maendeleo ya Mkonge kutoka TSB, Simon Kibasa, amesema Mkoa wa Dodoma bado uko kwenye hatua za awali za kilimo cha mkonge kutokana na wakulima wengi kuwa katika maandalizi au wameshapanda lakini hawajaanza kuvuna.

“Uzalishaji wa mkonge nchini umeongezeka kutoka tani 39,484 mwaka 2021 hadi kufikia tani 61,215 kwa sasa. Mkoa wa Tanga unaongoza kwa uzalishaji kwa takribani tani 34,000,” amesema Kibasa.

Ameongeza kuwa hamasa ya serikali na Bodi imechangia ongezeko la wakulima wapya katika maeneo mbalimbali, ikiwemo Dodoma.

“Kwa sasa kuna zaidi ya ekari 240 zinazolimwa mkonge Dodoma kutoka kwa wakulima waliotembelewa, na tunaamini zitaongezeka kwani bado kuna wakulima ambao hatujawafikia,” amesema.

Kibasa ameeleza kuwa kupitia maonesho hayo, wakulima watatu kutoka Dodoma wamejitokeza na kuomba kutembelewa kwa ajili ya usajili na bodi, na kwamba watafikiwa mara baada ya maonesho kumalizika.

spot_img

Latest articles

Makamu wa Rais atangaza kujiuzulu

Makamu wa Rais wa Tanzania, Balozi Dk. Emmanuel Nchimbi, ametangaza kujiuzulu wadhifa wake kuanzia...

RAIS SAMIA AAGIZA WAKUU WA MIKOA KUJIANDAA NA UDHIBITI WA ATHARI ZA ELNINO

Na Mwandishi Wetu RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan,...

Rais Samia azindua Kituo cha kuzalisha Umeme cha Julius Nyerere

Na Mwandishi Wetu RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan,...

JNHPP kuongeza Umeme wa Gridi ya Taifa kwa asilimia 45

Na Tatu Mohamed BWAWA la Julius Nyerere (JNHPP) linatarajiwa kuongeza kwa kiasi kikubwa uwezo...

More like this

Makamu wa Rais atangaza kujiuzulu

Makamu wa Rais wa Tanzania, Balozi Dk. Emmanuel Nchimbi, ametangaza kujiuzulu wadhifa wake kuanzia...

RAIS SAMIA AAGIZA WAKUU WA MIKOA KUJIANDAA NA UDHIBITI WA ATHARI ZA ELNINO

Na Mwandishi Wetu RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan,...

Rais Samia azindua Kituo cha kuzalisha Umeme cha Julius Nyerere

Na Mwandishi Wetu RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan,...