Katibu Mkuu Kiongozi kufungua mafunzo kwa watendaji wakuu taasisi za umma

Na mwandishi wa OMH, HDar es Salaam

KATIBU Mkuu Kiongozi, Balozi Dkt. Moses Kusiluka anatarajia kuwa mgeni rasmi katika ufunguzi wa mafunzo ya siku nne kwa watendaji wakuu wa taasisi, mashirika ya umma na wakala wa serikali.

Mafunzo hayo yatakayofanyika kuanzia Julai 28-31, 2025 katika shule ya uongozi ya Mwalimu Nyerere, Kibaha, mkoani Pwani, yanaratibiwa na Ofisi ya Msajili wa Hazina kwa kushirikiana na Taasisi ya Uongozi.

Lengo la mafunzo hayo kwa watendaji wakuu wapya na wale ambao hawajawahi kupatiwa mafunzo ni kuwajengea uwezo watendaji wakuu ili watekeleze majukumu yao kwa weledi na kwa kuzingatia misingi ya utawala bora.

Msajili wa Hazina, Nehemiah Mchechu Alhamisi, Julai 24, 2025, alisema Program ya mafunzo kwa watendaji wakuu ni kielelezo dhahiri cha dhamira ya dhati ya serikali ya awamu ya sita ya kuhakikisha kuwa watendaji wanajua nini wanatakiwa kwenda kufanya katika taasisi walizopewa kuongoza.

“Mafunzo haya yanayolenga kuongeza tija na ufanisi katika taasisi za umma, ni endelevu,” alisema Mchechu.

Ikumbukwe kwa mara ya kwanza mafunzo haya yalifanyika Oktoba 2024, Mchechu alisema kuwa programu hiyo ya mafunzo ni mwendelezo wa hatua mbalimbali ambazo Ofisi ya Msajili wa Hazina inachukua katika kutafsiri na kutekeleza kwa vitendo maono ya Mheshimwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania pamoja na falsafa ya 4Rs.

“Katika falsafa ya 4Rs tumejikita katika R mbili kati ya nne ambazo ni Reform (mabadiliko) na Rebuild (kujenga upya),” alisema.

Alifafanua: ”Hapa tutajikita zaidi katika eneo la kuwajengea uwezo watendaji wakuu ili wawe na ufanisi zaidi katika usimamizi wa taasisi za umma.”

Ofisi ya Msajili wa Hazina inasimamia jumla ya taasisi, mashirika ya umma, wakala wa serikali na kampuni ambazo serikali ina umiliki wa hisa chache 308, huku uwekezaji ukiwa n Sh86.25 trilioni.

Kati ya kiasi hicho Sh83.33 trilioni zimewekezwa kwenye taasisi, mashirika ya umma na wakala wa serikali, huku Sh2.92 trilioni zikiwekezwa kwenye kampuni ambazo serikali ina umiliki wa hisa chache.

spot_img

Latest articles

DCEA yakamata Lita 66,048 za kemikali bashirifu

NA MWANDISHI WETU MAMLAKA ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya ((DCEA), imefanikiwa kukamata...

Chevron yaonesha nia ya kuwekeza Tanzania katika sekta ndogo ya Mafuta na Gesi Asilia

Na Mwandishi Wetu KAMPUNI kubwa ya nishati kutoka Marekani, Chevron Corporation imeeleza utayari wake wa...

Jumba la maajabu laiponza Yanga,  yapigwa faini  milioni 30,  Meneja  matatani

Na Mwandishi Wetu KLABU ya Yanga imetozwa faini ya Sh 30 milioni  kwa kosa la...

Waziri Ndejembi atoa maelekezo mazito utekelezaji wa mradi Malagarasi MW 49.6 KIGOMA

📌Hajaridhishwa na kasi ya utekelezaji wa mkandarasi kwenye mradi 📌Aagiza ukaguzi maalum wa matumizi ya...

More like this

DCEA yakamata Lita 66,048 za kemikali bashirifu

NA MWANDISHI WETU MAMLAKA ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya ((DCEA), imefanikiwa kukamata...

Chevron yaonesha nia ya kuwekeza Tanzania katika sekta ndogo ya Mafuta na Gesi Asilia

Na Mwandishi Wetu KAMPUNI kubwa ya nishati kutoka Marekani, Chevron Corporation imeeleza utayari wake wa...

Jumba la maajabu laiponza Yanga,  yapigwa faini  milioni 30,  Meneja  matatani

Na Mwandishi Wetu KLABU ya Yanga imetozwa faini ya Sh 30 milioni  kwa kosa la...