Tanzania yaorodheshwa nafasi ya 19 Duniani kwa kushawishiwa na China – Ripoti Mpya

Na Mwandishi Wetu

TANZANIA imeshika nafasi ya 19 kati ya nchi 101 duniani zilizotathminiwa kuhusu kiwango cha ushawishi wa Jamhuri ya Watu wa China, kwa mujibu wa ripoti mpya ya China Index 2024 iliyotolewa na shirika la Doublethink Lab kupitia mtandao wa China in the World (CITW).

Ripoti hiyo ya kina inaonyesha kuwa ushawishi wa China nchini Tanzania umejikita zaidi katika maeneo ya kiuchumi, kijeshi, na kisera, huku nchi hizi mbili zikionekana kuwa na uhusiano wa karibu unaozidi kuimarika kila mwaka.

Katika eneo la ushirikiano wa kijeshi, Tanzania imepanda hadi nafasi ya 6 duniani, ikiashiria mahusiano ya kina ya kitaasisi kama vile mafunzo ya wanajeshi wa Tanzania nchini China, mazoezi ya pamoja kama Peace Unity-2024, pamoja na uhamishaji wa zana na teknolojia za kijeshi.

Aidha, katika sera za kigeni, Tanzania pia imeshika nafasi ya 6, ikiungwa mkono na msimamo wake wa wazi katika kuunga mkono sera kuu za China zikiwemo One China Principle, na masuala ya Taiwan, Hong Kong, na Xinjiang.

Kwa mujibu wa ripoti hiyo, Tanzania imeshika nafasi ya 9 katika kundi la Rule-Making Cluster linalohusisha masuala ya kijeshi, sheria na sera za nje, ikiwa ni kielelezo cha mafanikio ya China katika kujenga ushawishi wake wa kidiplomasia na kiusalama kupitia ushirikiano wa kiuchumi.

Ripoti hiyo imeeleza ushahidi unaonesha kuwa Shule ya Uongozi ya Mwalimu Julius Nyerere huko Kibaha ni jukwaa muhimu kwa ajili ya mafunzo ya viongozi wa serikali.

Kupitia shule hiyo, China hupata nafasi ya kuimarisha mahusiano na viongozi wa Tanzania kupitia diplomasia ya “chama kwa chama.”

Ushahidi huu wote umetolewa na wadau wa kikanda wa China Index, ambapo katika kesi hii ni mchambuzi wa masuala ya siasa, mwandishi na mtafiti Emeka Umejei, na baadaye kuthibitishwa na wataalamu wa ndani ya nchi.

Utafiti huu wa mwaka 2024 umefanywa na wachambuzi huru kwa kushirikiana na watafiti wa ndani na kimataifa.

Ripoti kamili ya China Index 2024 inatarajiwa kupatikana hivi karibuni kwa matumizi ya umma. Hata hivyo, data za awali tayari zinapatikana kwa watafiti, watunga sera na wanahabari wanaopenda kuchambua zaidi mwenendo wa ushawishi wa China duniani.

spot_img

Latest articles

Mchezo wa kuogelea wazidi kupaa nchini, TSA  yafichua siri

Na Winfrida  Mtoi MCHEZO wa kuogelea umezidi kushika kasi nchini  kutokana na kuongezeka idadi ya...

Dkt Nchimbi atembelea banda la Tanesco

Na Mwandishi Wetu MAKAMU wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Balozi...

Waogeleaji chipukizi 400 kutikisa Dar kesho

Na Mwandishi Wetu Zaidi ya waogeleaji 400 wenye umri wa miaka 6 hadi 12 wanatarajiwa...

Wabunge walifuata mkumbo kwenda Morocco kuishangilia Serengeti Boys lawakuta jambo

Na Mwandishi Wetu SPIKA wa Mbunge la Tanzania, Mussa Azzan Zungu ametoa siku nne za...

More like this

Mchezo wa kuogelea wazidi kupaa nchini, TSA  yafichua siri

Na Winfrida  Mtoi MCHEZO wa kuogelea umezidi kushika kasi nchini  kutokana na kuongezeka idadi ya...

Dkt Nchimbi atembelea banda la Tanesco

Na Mwandishi Wetu MAKAMU wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Balozi...

Waogeleaji chipukizi 400 kutikisa Dar kesho

Na Mwandishi Wetu Zaidi ya waogeleaji 400 wenye umri wa miaka 6 hadi 12 wanatarajiwa...