Tanzania yaorodheshwa nafasi ya 19 Duniani kwa kushawishiwa na China – Ripoti Mpya

Na Mwandishi Wetu

TANZANIA imeshika nafasi ya 19 kati ya nchi 101 duniani zilizotathminiwa kuhusu kiwango cha ushawishi wa Jamhuri ya Watu wa China, kwa mujibu wa ripoti mpya ya China Index 2024 iliyotolewa na shirika la Doublethink Lab kupitia mtandao wa China in the World (CITW).

Ripoti hiyo ya kina inaonyesha kuwa ushawishi wa China nchini Tanzania umejikita zaidi katika maeneo ya kiuchumi, kijeshi, na kisera, huku nchi hizi mbili zikionekana kuwa na uhusiano wa karibu unaozidi kuimarika kila mwaka.

Katika eneo la ushirikiano wa kijeshi, Tanzania imepanda hadi nafasi ya 6 duniani, ikiashiria mahusiano ya kina ya kitaasisi kama vile mafunzo ya wanajeshi wa Tanzania nchini China, mazoezi ya pamoja kama Peace Unity-2024, pamoja na uhamishaji wa zana na teknolojia za kijeshi.

Aidha, katika sera za kigeni, Tanzania pia imeshika nafasi ya 6, ikiungwa mkono na msimamo wake wa wazi katika kuunga mkono sera kuu za China zikiwemo One China Principle, na masuala ya Taiwan, Hong Kong, na Xinjiang.

Kwa mujibu wa ripoti hiyo, Tanzania imeshika nafasi ya 9 katika kundi la Rule-Making Cluster linalohusisha masuala ya kijeshi, sheria na sera za nje, ikiwa ni kielelezo cha mafanikio ya China katika kujenga ushawishi wake wa kidiplomasia na kiusalama kupitia ushirikiano wa kiuchumi.

Ripoti hiyo imeeleza ushahidi unaonesha kuwa Shule ya Uongozi ya Mwalimu Julius Nyerere huko Kibaha ni jukwaa muhimu kwa ajili ya mafunzo ya viongozi wa serikali.

Kupitia shule hiyo, China hupata nafasi ya kuimarisha mahusiano na viongozi wa Tanzania kupitia diplomasia ya “chama kwa chama.”

Ushahidi huu wote umetolewa na wadau wa kikanda wa China Index, ambapo katika kesi hii ni mchambuzi wa masuala ya siasa, mwandishi na mtafiti Emeka Umejei, na baadaye kuthibitishwa na wataalamu wa ndani ya nchi.

Utafiti huu wa mwaka 2024 umefanywa na wachambuzi huru kwa kushirikiana na watafiti wa ndani na kimataifa.

Ripoti kamili ya China Index 2024 inatarajiwa kupatikana hivi karibuni kwa matumizi ya umma. Hata hivyo, data za awali tayari zinapatikana kwa watafiti, watunga sera na wanahabari wanaopenda kuchambua zaidi mwenendo wa ushawishi wa China duniani.

spot_img

Latest articles

Yanga kuikabili TRA bila Depu, kocha aeleza ugumu ulipo

Na Mwandishi Wetu WAKATI Yanga ikitarajiwa kushuka dimbani kesho Machi 18, 2026  kuikabili TRA United katika Ligi...

Vijana 3,967 waomba uwezeshaji kupitia Go Green na IMBEJU ya CRDB Bank Foundation

Na Mwandishi wetu JUMLA ya vijana 3,967 kutoka maeneo mbalimbali nchini wamewasilisha maombi ya...

RC Kunenge aipongeza Dawasa, awapa jukumu madiwani

Na Mwandishi wetu MKUU wa Mkoa wa Pwani, Abubakar Kunenge amesema ushirikishwaji wananchi kwenye...

Serikali yatoa maelekezo nane kuimarisha kampuni ambazo ina umiliki hisa chache kuelekea Dira 2050

Na Mwandishi wetu, Arusha SERIKALI imetoa maelekezo nane ya kimkakati yanayolenga kuimarisha utendaji wa kampuni...

More like this

Yanga kuikabili TRA bila Depu, kocha aeleza ugumu ulipo

Na Mwandishi Wetu WAKATI Yanga ikitarajiwa kushuka dimbani kesho Machi 18, 2026  kuikabili TRA United katika Ligi...

Vijana 3,967 waomba uwezeshaji kupitia Go Green na IMBEJU ya CRDB Bank Foundation

Na Mwandishi wetu JUMLA ya vijana 3,967 kutoka maeneo mbalimbali nchini wamewasilisha maombi ya...

RC Kunenge aipongeza Dawasa, awapa jukumu madiwani

Na Mwandishi wetu MKUU wa Mkoa wa Pwani, Abubakar Kunenge amesema ushirikishwaji wananchi kwenye...