Kambi ya kutengeneza mishipa ya damu, upandikizaji Figo yaanza rasmi Muhimbili -Mloganzila

Na Mwandishi Wetu

HOSPITALI ya Taifa Muhimbili-Mloganzila imeanza kambi maalum ya kutengeneza mishipa ya kuchuja damu sambamba na kupandikiza figo kwa wagonjwa wenye changamoto za figo ambayo itahitimishwa rasmi Julai 23, 2025.

Kambi hiyo inafanywa na wataalam wa Muhimbili Mloganzila kwa kushirikiana na jopo la wataalam kutoka Korea Kusini linalo ongozwa na Prof. Park Kwan Tae ambaye ni Daktari Bingwa Bobezi wa Upasuaji chini ya uaratibu wa Taasisi ya Africa Future Foundation (AFF) ya nchini Korea Kusini.

Upandikizaji wa figo unafanyika kwa kuvuna figo kutoka kwa mchangiaji kwa kutumia matundu madogo (Laparascopic Hand Assisted Donor Nephroctomy) utaalam ambao kwa hapa nchini unapatikana Hospitali ya Taifa Muhimbili Mloganzila pekee.

Aidha,wataalam mbalimbali kutoka ndani na nje ya nchi wanajengewa uwezo wa kutoa huduma hizo katika maeneo yao ili kuwapunguzia wananchi usumbufu wa kwenda mbali na maeneo yao kufuata huduma hizo.

Hadi kuhitimishwa kwa kambi hiyo wananchi takribani 60 watanufaika na huduma za kutengenezewa mishipa ya kuchuja damu na wananchi wanne watapandikizwa figo na kufikisha idadi ya wanufaika waliopandikizwa figo kufikia 19 tangu huduma hizo zilipoanza rasmi katika hospitali hiyo mwaka 2023.

spot_img

Latest articles

Mwakinyo kuilipia kisasi Taifa Stars dhidi ya Mnigeria kesho, Furahi apania rekodi

Na Winfrida Mtoi BONDIA wa kimataifa wa Tanzania, Hassan Mwakinyo, ameweka bayana kuwa pambano lake...

Serikali kuendelea kuwawezesha vijana kijamii, kiuchumi

Na Tatu Mohamed WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Rais – Maendeleo ya Vijana, Joel...

Kids Holiday Festival yawavuta mamia ya watoto, CRDB yatumia jukwaa kujenga uelewa wa fedha

Na Mwandishi Wetu BURUDANI na michezo mbalimbali vilitawala Tamasha la Kids Holiday Festival lililowakusanya...

Mambo: Demokrasia haijengwi kwa mashinikizo, vitisho

Na Mwandishi Wetu ALIYEKUWA Mgombea wa Bavicha Taifa, Masoud Mambo amesema kuwa demokrasia ya...

More like this

Mwakinyo kuilipia kisasi Taifa Stars dhidi ya Mnigeria kesho, Furahi apania rekodi

Na Winfrida Mtoi BONDIA wa kimataifa wa Tanzania, Hassan Mwakinyo, ameweka bayana kuwa pambano lake...

Serikali kuendelea kuwawezesha vijana kijamii, kiuchumi

Na Tatu Mohamed WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Rais – Maendeleo ya Vijana, Joel...

Kids Holiday Festival yawavuta mamia ya watoto, CRDB yatumia jukwaa kujenga uelewa wa fedha

Na Mwandishi Wetu BURUDANI na michezo mbalimbali vilitawala Tamasha la Kids Holiday Festival lililowakusanya...