Ally Kamwe akiri kuvutiwa na Tshabalala

Na Mwandishi Wetu

Ofisa Habari wa klabu  ya Yanga Ally  Kamwe amesema licha ya kuwa yupo upande mwingine lakini  ni shabiki mkubwa wa wachezaji  wa Simba, Mohammed Hussein ‘Tshabalala na Shomari Kapombe kutokana na  uwezo mkubwa wa nyota hao.

Kamwe ametoa kauli hiyo kipindi ambacho kuna  na tetesi kuwa Yanga wanaitaka saini ya Tshabalala  katika kuimarisha kikosi chao.

“Nchi hii hapa  hakuna mwanadamu anaweza akadharau uwezo wa Mohamed Hussein Zimbwe na Shomari Kapombe, Mimi mwenyewe ni shabiki mkubwa wa hao watu wawili ni wachezaji wazuri,” amesema Kamwe.

Hata hivyo Kamwe hajaweka wazi kuwa klabu hiyo inamhitaji mchezaji huyo baada ya kusema bado hawajaanza usajili wala kutoa orodha ya wachezaji wanaoondoka klabuni hapo.

“Kuanzia tarehe 20 mwezi huu ndiyo  Yanga tutaanza kutoa taarifa rasmi ya nani katoka nani kaingia, sisi hatuna mambo ya ‘Thank You’ kipindi hiki,” amesema Kamwe.

spot_img

Latest articles

Arajiga kuchezesha CHAN

Na Mwandishi Wetu Mwamuzi  wa Tanzania  ,Ahmed Arajiga  ni miongoni  mwa waamuzi wa  wameteuliwa  kuchezesha michuano ya  CHAN yanayotarajiwa kuanza kutimua vumbi...

Rais Samia atoa  wito utekelezaji Dira ya Taifa 2050, asema Dk. Mpango hatapumzika

Na Mwandishi Wetu Rais Samia Suluhu Hassan, amezindua rasmi Dira ya Taifa ya Maendeleo ya...

Rostam: Hatuwezi kufanikiwa kwa kuwatenga wafanyabiashara wa ndani na kutegemea wageni

Na Mwandishi Wetu MFANYABIASHARA maarufu na mwakilishi wa sekta binafsi, Rostam Azizi, amesema kuwa...

Jaji Mkuu Masaju amepita mlemle

JAJI Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, George Mcheche Masaju amemaliza mwezi mmoja...

More like this

Arajiga kuchezesha CHAN

Na Mwandishi Wetu Mwamuzi  wa Tanzania  ,Ahmed Arajiga  ni miongoni  mwa waamuzi wa  wameteuliwa  kuchezesha michuano ya  CHAN yanayotarajiwa kuanza kutimua vumbi...

Rais Samia atoa  wito utekelezaji Dira ya Taifa 2050, asema Dk. Mpango hatapumzika

Na Mwandishi Wetu Rais Samia Suluhu Hassan, amezindua rasmi Dira ya Taifa ya Maendeleo ya...

Rostam: Hatuwezi kufanikiwa kwa kuwatenga wafanyabiashara wa ndani na kutegemea wageni

Na Mwandishi Wetu MFANYABIASHARA maarufu na mwakilishi wa sekta binafsi, Rostam Azizi, amesema kuwa...