Ally Kamwe akiri kuvutiwa na Tshabalala

Na Mwandishi Wetu

Ofisa Habari wa klabu  ya Yanga Ally  Kamwe amesema licha ya kuwa yupo upande mwingine lakini  ni shabiki mkubwa wa wachezaji  wa Simba, Mohammed Hussein ‘Tshabalala na Shomari Kapombe kutokana na  uwezo mkubwa wa nyota hao.

Kamwe ametoa kauli hiyo kipindi ambacho kuna  na tetesi kuwa Yanga wanaitaka saini ya Tshabalala  katika kuimarisha kikosi chao.

“Nchi hii hapa  hakuna mwanadamu anaweza akadharau uwezo wa Mohamed Hussein Zimbwe na Shomari Kapombe, Mimi mwenyewe ni shabiki mkubwa wa hao watu wawili ni wachezaji wazuri,” amesema Kamwe.

Hata hivyo Kamwe hajaweka wazi kuwa klabu hiyo inamhitaji mchezaji huyo baada ya kusema bado hawajaanza usajili wala kutoa orodha ya wachezaji wanaoondoka klabuni hapo.

“Kuanzia tarehe 20 mwezi huu ndiyo  Yanga tutaanza kutoa taarifa rasmi ya nani katoka nani kaingia, sisi hatuna mambo ya ‘Thank You’ kipindi hiki,” amesema Kamwe.

spot_img

Latest articles

Waziri wa Nishati Ndejembi azindua rasmi mita janja

Na Mwandishi Wetu WAZIRI wa Nishati, Deogratius Ndejembi amezindua rasmi mita janja (smart meter)...

RC Kunenge: Mto Ruvu ubaki kwa matumizi ya binadamu tu, tusitishe shughuli nyingine kwa muda

Na Mwandishi Wetu MKUU wa Mkoa wa Pwani, Abubakar Kunenge, ametoa wito kwa wakulima...

Tume ya Jaji Chande na mlima wenye utelezi

KAMA kuna tume ya uchunguzi iliyopata kuundwa nchini kwa jambo mahususi, ikajikuta katika uwanja...

Rais Samia: Walilenga kupindua dola

RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, amesema kuwa vurugu...

More like this

Waziri wa Nishati Ndejembi azindua rasmi mita janja

Na Mwandishi Wetu WAZIRI wa Nishati, Deogratius Ndejembi amezindua rasmi mita janja (smart meter)...

RC Kunenge: Mto Ruvu ubaki kwa matumizi ya binadamu tu, tusitishe shughuli nyingine kwa muda

Na Mwandishi Wetu MKUU wa Mkoa wa Pwani, Abubakar Kunenge, ametoa wito kwa wakulima...

Tume ya Jaji Chande na mlima wenye utelezi

KAMA kuna tume ya uchunguzi iliyopata kuundwa nchini kwa jambo mahususi, ikajikuta katika uwanja...