Ndumbaro: Sheria 300 Zimetafsiriwa kwa Kiswahili Ili Kuimarisha Uelewa kwa Wananchi

Na Tatu Mohamed

WAZIRI wa Katiba na Sheria, Dkt. Damas Ndumbaro, amesema kuwa hadi kufikia Juni 30, 2025, tayari Sheria 300 kati ya 446 zimetafsiriwa kutoka Kiingereza kwenda Kiswahili na Ofisi ya Mwandishi Mkuu wa Sheria (OCPD), ikiwa ni juhudi za serikali kuhakikisha Watanzania wanaelewa sheria zinazowaongoza.

Akizungumza jana jijini Dar es Salaam alipotembelea banda la OCPD katika Maonesho ya 49 ya Biashara ya Kimataifa (Sabasaba), Dk. Ndumbaro alisema serikali imetenga bajeti mahsusi kwa ajili ya kutafsiri sheria 146 zilizobaki.

“Ni muhimu Watanzania waweze kuelewa sheria kwa lugha wanayoitumia kila siku. Hii ndiyo maana tunasisitiza tafsiri ya sheria kwa Kiswahili,” alisema.

Alibainisha kuwa Ofisi ya Mwandishi Mkuu wa Sheria ni kiungo muhimu katika mchakato mzima wa utungaji, marekebisho na ufasili wa sheria kabla hazijawasilishwa bungeni.

“Bila ofisi hii, hakuna sheria inayotungwa au kufanyiwa marekebisho. Iwapo sheria zitakuwa na makosa, hata mahakama inaweza kutoa maamuzi yasiyo sahihi,” aliongeza.

Aidha, Dk. Ndumbaro alisema hatua ya kutafsiri sheria kwa Kiswahili inalenga kuwasaidia wananchi wa kawaida, wakiwemo wanafunzi na wanasheria, kuelewa vyema misingi ya sheria nchini.

spot_img

Latest articles

Mwakinyo kuilipia kisasi Taifa Stars dhidi ya Mnigeria kesho, Furahi apania rekodi

Na Winfrida Mtoi BONDIA wa kimataifa wa Tanzania, Hassan Mwakinyo, ameweka bayana kuwa pambano lake...

Serikali kuendelea kuwawezesha vijana kijamii, kiuchumi

Na Tatu Mohamed WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Rais – Maendeleo ya Vijana, Joel...

Kids Holiday Festival yawavuta mamia ya watoto, CRDB yatumia jukwaa kujenga uelewa wa fedha

Na Mwandishi Wetu BURUDANI na michezo mbalimbali vilitawala Tamasha la Kids Holiday Festival lililowakusanya...

Mambo: Demokrasia haijengwi kwa mashinikizo, vitisho

Na Mwandishi Wetu ALIYEKUWA Mgombea wa Bavicha Taifa, Masoud Mambo amesema kuwa demokrasia ya...

More like this

Mwakinyo kuilipia kisasi Taifa Stars dhidi ya Mnigeria kesho, Furahi apania rekodi

Na Winfrida Mtoi BONDIA wa kimataifa wa Tanzania, Hassan Mwakinyo, ameweka bayana kuwa pambano lake...

Serikali kuendelea kuwawezesha vijana kijamii, kiuchumi

Na Tatu Mohamed WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Rais – Maendeleo ya Vijana, Joel...

Kids Holiday Festival yawavuta mamia ya watoto, CRDB yatumia jukwaa kujenga uelewa wa fedha

Na Mwandishi Wetu BURUDANI na michezo mbalimbali vilitawala Tamasha la Kids Holiday Festival lililowakusanya...