Ndumbaro: Sheria 300 Zimetafsiriwa kwa Kiswahili Ili Kuimarisha Uelewa kwa Wananchi

Na Tatu Mohamed

WAZIRI wa Katiba na Sheria, Dkt. Damas Ndumbaro, amesema kuwa hadi kufikia Juni 30, 2025, tayari Sheria 300 kati ya 446 zimetafsiriwa kutoka Kiingereza kwenda Kiswahili na Ofisi ya Mwandishi Mkuu wa Sheria (OCPD), ikiwa ni juhudi za serikali kuhakikisha Watanzania wanaelewa sheria zinazowaongoza.

Akizungumza jana jijini Dar es Salaam alipotembelea banda la OCPD katika Maonesho ya 49 ya Biashara ya Kimataifa (Sabasaba), Dk. Ndumbaro alisema serikali imetenga bajeti mahsusi kwa ajili ya kutafsiri sheria 146 zilizobaki.

“Ni muhimu Watanzania waweze kuelewa sheria kwa lugha wanayoitumia kila siku. Hii ndiyo maana tunasisitiza tafsiri ya sheria kwa Kiswahili,” alisema.

Alibainisha kuwa Ofisi ya Mwandishi Mkuu wa Sheria ni kiungo muhimu katika mchakato mzima wa utungaji, marekebisho na ufasili wa sheria kabla hazijawasilishwa bungeni.

“Bila ofisi hii, hakuna sheria inayotungwa au kufanyiwa marekebisho. Iwapo sheria zitakuwa na makosa, hata mahakama inaweza kutoa maamuzi yasiyo sahihi,” aliongeza.

Aidha, Dk. Ndumbaro alisema hatua ya kutafsiri sheria kwa Kiswahili inalenga kuwasaidia wananchi wa kawaida, wakiwemo wanafunzi na wanasheria, kuelewa vyema misingi ya sheria nchini.

spot_img

Latest articles

ELAF yahimiza maridhiano na amani baada ya Uchaguzi Mkuu

Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam TAASISI ya Everlasting Legal Aid Foundation (ELAF) imewataka Watanzania...

Taifa Stars ya Gamondi amrejesha Kelvin John

Na Mwandishi Wetu Kaimu Kocha Mkuu wa timu ya Taifa, Taifa Stars Miguel Gamondi amemrudisha...

‘Hali ya huduma ya maji Dar, Pwani ni shwari’

Na Mwandishi Wetu WAKAZI mbalimbali wa Jiji la Dar es Salaam na Mkoa wa...

Mwanasheria Mkuu wa Serikali: Uchaguzi Mkuu wa 2025 ni halali

Na Mwandishi wetu MWANASHERIA Mkuu wa Serikali, Hamza Johari amesema kuwa, Uchaguzi Mkuu wa...

More like this

ELAF yahimiza maridhiano na amani baada ya Uchaguzi Mkuu

Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam TAASISI ya Everlasting Legal Aid Foundation (ELAF) imewataka Watanzania...

Taifa Stars ya Gamondi amrejesha Kelvin John

Na Mwandishi Wetu Kaimu Kocha Mkuu wa timu ya Taifa, Taifa Stars Miguel Gamondi amemrudisha...

‘Hali ya huduma ya maji Dar, Pwani ni shwari’

Na Mwandishi Wetu WAKAZI mbalimbali wa Jiji la Dar es Salaam na Mkoa wa...