Tyson wa Bongo afunga mtaa 

Na  Winfrida  Mtoi

Bondia wa ngumi za kulipwa Hassan Ndonga maarufu Tyson wa Bongo amefunga  Mtaa wa Banda Mabibo, Dar es Salaam kutokana na wingi wa mashabiki waliojitokeza kumsapoti katika maandalizi ya pambano lake la  Dar Boxing Derby  dhidi ya Mohammed Mpombo  litakalofanyika Julai 26,2025, Viwanja Vya Leaders Club. 

Tyson ambaye anatokea kambi ya Makatuni Pesa, ameweka wazi kuwa hajawahi kufeli katika mapambano yake mengi aliyocheza na kuwahakikishia ushindi mashabiki zake.

“Ukizungumzia K.O huwa inakuja yenyewe ‘automatic, sababu hata ukiangalia mapambano yangu mawili ya mwisho,  la kwanza nilikuwa nacheza raundi nane lakini nikampiga mtu  raundi ya pili, jingine nilicheza Morogoro katika raundi nane nikampiga mpinzani wangu katika raundi ya sita,” ametamba.

Amewaambia mashabiki zake wasisite kujitokeza siku hiyo kwa kuhofia kwani yeye amejipanga  kushinda kutokana na maandalizi anayofanya.

Mmoja wa mashabiki wa bondia huyo,  Hamza. Mohammed, amesema anamkubali bondia wao kwa sababu siku zote hawana kazi mbovu na ameshuhudia hilo mazoezini  na ulingo utasema siku hiyo.

spot_img

Latest articles

Waziri wa Nishati Ndejembi azindua rasmi mita janja

Na Mwandishi Wetu WAZIRI wa Nishati, Deogratius Ndejembi amezindua rasmi mita janja (smart meter)...

RC Kunenge: Mto Ruvu ubaki kwa matumizi ya binadamu tu, tusitishe shughuli nyingine kwa muda

Na Mwandishi Wetu MKUU wa Mkoa wa Pwani, Abubakar Kunenge, ametoa wito kwa wakulima...

Tume ya Jaji Chande na mlima wenye utelezi

KAMA kuna tume ya uchunguzi iliyopata kuundwa nchini kwa jambo mahususi, ikajikuta katika uwanja...

Rais Samia: Walilenga kupindua dola

RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, amesema kuwa vurugu...

More like this

Waziri wa Nishati Ndejembi azindua rasmi mita janja

Na Mwandishi Wetu WAZIRI wa Nishati, Deogratius Ndejembi amezindua rasmi mita janja (smart meter)...

RC Kunenge: Mto Ruvu ubaki kwa matumizi ya binadamu tu, tusitishe shughuli nyingine kwa muda

Na Mwandishi Wetu MKUU wa Mkoa wa Pwani, Abubakar Kunenge, ametoa wito kwa wakulima...

Tume ya Jaji Chande na mlima wenye utelezi

KAMA kuna tume ya uchunguzi iliyopata kuundwa nchini kwa jambo mahususi, ikajikuta katika uwanja...