TPDC yapata Tuzo ya Taasisi Bora Sabasaba kwa miaka mitano mfululizo

Na Tatu Mohamed

SHIRIKA la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC) limeandika historia kwa kutwaa tuzo ya Taasisi Bora za Umma katika Maonesho ya 49 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam (Sabasaba), ikiwa ni mara ya tano mfululizo kushinda tuzo hiyo kutokana na ubora wa huduma na uwajibikaji wake kwa wananchi.

Tuzo hiyo imetolewa kama uthibitisho wa mchango wa TPDC katika kuimarisha uwazi, ubunifu na utoaji wa huduma bora ndani ya sekta ya nishati nchini.

Mgeni rasmi katika hafla hiyo ya ufunguzi alikuwa Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dkt. Hussein Ali Mwinyi.

Akizungumza mara baada ya kupokea tuzo hiyo, Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano wa TPDC, Maria Mselemu, alisema kuwa mafanikio hayo ni matokeo ya utendaji kazi bora, nidhamu ya kiutendaji na ufuatiliaji wa karibu wa miradi inayosimamiwa na shirika hilo.

“Hii ni tuzo yetu ya tano mfululizo katika maonesho ya Sabasaba. Ubora wa huduma zetu, miradi ya kimkakati na mchango wetu katika utunzaji wa mazingira umekuwa na mchango mkubwa katika mafanikio haya,” alisema Mselemu.

Aliongeza kuwa TPDC imefanikiwa kwa kiasi kikubwa kupunguza utoaji wa hewa ukaa kwa kuhimiza matumizi ya nishati safi, hususan kwa matumizi ya majumbani na kwenye magari.

“Tayari tumeondoa zaidi ya tani 100,000 za hewa ukaa kupitia juhudi zetu za kusambaza gesi asilia. Ni mafanikio makubwa katika mapambano dhidi ya mabadiliko ya tabianchi,” alieleza.

TPDC pia imewahi kutwaa tuzo ya mazingira kutokana na juhudi zake katika kulinda na kuhifadhi mazingira kupitia matumizi ya nishati mbadala, jambo linaloendelea kuipa heshima shirika hilo miongoni mwa taasisi za umma.

Maonesho ya Sabasaba yameendelea kuwa jukwaa muhimu la kuonesha ubunifu, huduma na bidhaa bora kwa Watanzania, huku yakitoa fursa kwa mashirika kama TPDC kushirikiana na wadau wa maendeleo kutoka ndani na nje ya nchi.

spot_img

Latest articles

Yanga kuikabili TRA bila Depu, kocha aeleza ugumu ulipo

Na Mwandishi Wetu WAKATI Yanga ikitarajiwa kushuka dimbani kesho Machi 18, 2026  kuikabili TRA United katika Ligi...

Vijana 3,967 waomba uwezeshaji kupitia Go Green na IMBEJU ya CRDB Bank Foundation

Na Mwandishi wetu JUMLA ya vijana 3,967 kutoka maeneo mbalimbali nchini wamewasilisha maombi ya...

RC Kunenge aipongeza Dawasa, awapa jukumu madiwani

Na Mwandishi wetu MKUU wa Mkoa wa Pwani, Abubakar Kunenge amesema ushirikishwaji wananchi kwenye...

Serikali yatoa maelekezo nane kuimarisha kampuni ambazo ina umiliki hisa chache kuelekea Dira 2050

Na Mwandishi wetu, Arusha SERIKALI imetoa maelekezo nane ya kimkakati yanayolenga kuimarisha utendaji wa kampuni...

More like this

Yanga kuikabili TRA bila Depu, kocha aeleza ugumu ulipo

Na Mwandishi Wetu WAKATI Yanga ikitarajiwa kushuka dimbani kesho Machi 18, 2026  kuikabili TRA United katika Ligi...

Vijana 3,967 waomba uwezeshaji kupitia Go Green na IMBEJU ya CRDB Bank Foundation

Na Mwandishi wetu JUMLA ya vijana 3,967 kutoka maeneo mbalimbali nchini wamewasilisha maombi ya...

RC Kunenge aipongeza Dawasa, awapa jukumu madiwani

Na Mwandishi wetu MKUU wa Mkoa wa Pwani, Abubakar Kunenge amesema ushirikishwaji wananchi kwenye...