Wagombea  urais watano TFF wapigwa chini abaki  Karia 

Na Mwandishi Wetu

Kamati ya Uchaguzi ya TFF imewang’oa wagombea watano wa nafasi ya Urais wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) na kubaki mmoja ambaye ni Wallace Karia anayetetea kiti hicho.

Akitangaza ripoti ya usahili wa uchaguzi huo Mwenyekiti wa Kamati ya Uchaguzi wa TFF, Wakili Kiomoni Kibamba, amesema Karia ndiye mgombea pekee aliyekidhi vigezo na kwa mujibu wa Kanuni na kama kuna mtu anapingamizi bado ana nafasi ya kufanya hivyo.

“Kwenye nafasi ya urais kulikuwa na wagombea sita, mmoja hakutokea kwenye usahili na wengine wanne hawakukidhi matakwa ya kikanuni, mgombea mmoja amekidhi matakwa yote ya kikanuni na tumempitisha ambaye ni Wallace Karia,”amesema Kibamba.

Kibamba ameeleza kuwa kwenye nafasi ya wagombea wa nafasi ya ujumbe kulikuwa na wagombea 19 ambapo 17 walihudhuria usahili, saba wamekosa vigezo na kumi wamepitishwa kuendelea na mchakato wa uchaguzi katika hatua inayofuata.

spot_img

Latest articles

DCEA yakamata Lita 66,048 za kemikali bashirifu

NA MWANDISHI WETU MAMLAKA ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya ((DCEA), imefanikiwa kukamata...

Chevron yaonesha nia ya kuwekeza Tanzania katika sekta ndogo ya Mafuta na Gesi Asilia

Na Mwandishi Wetu KAMPUNI kubwa ya nishati kutoka Marekani, Chevron Corporation imeeleza utayari wake wa...

Jumba la maajabu laiponza Yanga,  yapigwa faini  milioni 30,  Meneja  matatani

Na Mwandishi Wetu KLABU ya Yanga imetozwa faini ya Sh 30 milioni  kwa kosa la...

Waziri Ndejembi atoa maelekezo mazito utekelezaji wa mradi Malagarasi MW 49.6 KIGOMA

📌Hajaridhishwa na kasi ya utekelezaji wa mkandarasi kwenye mradi 📌Aagiza ukaguzi maalum wa matumizi ya...

More like this

DCEA yakamata Lita 66,048 za kemikali bashirifu

NA MWANDISHI WETU MAMLAKA ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya ((DCEA), imefanikiwa kukamata...

Chevron yaonesha nia ya kuwekeza Tanzania katika sekta ndogo ya Mafuta na Gesi Asilia

Na Mwandishi Wetu KAMPUNI kubwa ya nishati kutoka Marekani, Chevron Corporation imeeleza utayari wake wa...

Jumba la maajabu laiponza Yanga,  yapigwa faini  milioni 30,  Meneja  matatani

Na Mwandishi Wetu KLABU ya Yanga imetozwa faini ya Sh 30 milioni  kwa kosa la...