Wagombea  urais watano TFF wapigwa chini abaki  Karia 

Na Mwandishi Wetu

Kamati ya Uchaguzi ya TFF imewang’oa wagombea watano wa nafasi ya Urais wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) na kubaki mmoja ambaye ni Wallace Karia anayetetea kiti hicho.

Akitangaza ripoti ya usahili wa uchaguzi huo Mwenyekiti wa Kamati ya Uchaguzi wa TFF, Wakili Kiomoni Kibamba, amesema Karia ndiye mgombea pekee aliyekidhi vigezo na kwa mujibu wa Kanuni na kama kuna mtu anapingamizi bado ana nafasi ya kufanya hivyo.

“Kwenye nafasi ya urais kulikuwa na wagombea sita, mmoja hakutokea kwenye usahili na wengine wanne hawakukidhi matakwa ya kikanuni, mgombea mmoja amekidhi matakwa yote ya kikanuni na tumempitisha ambaye ni Wallace Karia,”amesema Kibamba.

Kibamba ameeleza kuwa kwenye nafasi ya wagombea wa nafasi ya ujumbe kulikuwa na wagombea 19 ambapo 17 walihudhuria usahili, saba wamekosa vigezo na kumi wamepitishwa kuendelea na mchakato wa uchaguzi katika hatua inayofuata.

spot_img

Latest articles

Waziri wa Nishati Ndejembi azindua rasmi mita janja

Na Mwandishi Wetu WAZIRI wa Nishati, Deogratius Ndejembi amezindua rasmi mita janja (smart meter)...

RC Kunenge: Mto Ruvu ubaki kwa matumizi ya binadamu tu, tusitishe shughuli nyingine kwa muda

Na Mwandishi Wetu MKUU wa Mkoa wa Pwani, Abubakar Kunenge, ametoa wito kwa wakulima...

Tume ya Jaji Chande na mlima wenye utelezi

KAMA kuna tume ya uchunguzi iliyopata kuundwa nchini kwa jambo mahususi, ikajikuta katika uwanja...

Rais Samia: Walilenga kupindua dola

RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, amesema kuwa vurugu...

More like this

Waziri wa Nishati Ndejembi azindua rasmi mita janja

Na Mwandishi Wetu WAZIRI wa Nishati, Deogratius Ndejembi amezindua rasmi mita janja (smart meter)...

RC Kunenge: Mto Ruvu ubaki kwa matumizi ya binadamu tu, tusitishe shughuli nyingine kwa muda

Na Mwandishi Wetu MKUU wa Mkoa wa Pwani, Abubakar Kunenge, ametoa wito kwa wakulima...

Tume ya Jaji Chande na mlima wenye utelezi

KAMA kuna tume ya uchunguzi iliyopata kuundwa nchini kwa jambo mahususi, ikajikuta katika uwanja...