Dkt. Kimambo: Maafisa Ustawi wa Jamii Muhimbili zingatieni weledi, upendo na moyo wa huruma kwa wagonjwa

Na Mwandishi Wetu

MKURUGENZI Mtendaji wa Hospitali ya Taifa Muhimbili,(MNH) Dkt. Delilah Kimambo, amewataka watumishi wa ustawi wa jamii hospitalini hapo kuzingatia weledi na kuonyesha moyo wa huruma na upendo wakati wa kuwahudumia wateja wanaofika kupatiwa huduma katika ofisi zao.

Dkt. Kimambo ameyasema hayo leo Juni 27, 2025, wakati wa kikao cha pamoja na wafanyakazi wa idara hiyo, ikiwa ni sehemu ya mpango wake wa kuboresha mawasiliano ya ndani na kufanikisha uwajibikaji na uwazi katika utoaji wa huduma.

“Tujishushe kwenye viwango vya hawa watu, tuwahudumie kwa kujali na kwa upendo. Tutajua kwa kina shida zao na jinsi ya kuwasaidia kuendana na mahitaji yao. Nyie ni kitengo muhimu sana, nyie ndio watetezi wa wateja wetu, mnatakiwa kuwa sauti yao pale wanapokosa nguvu, na kuwa faraja yao pale wanapokata tamaa,” amesema Dkt. Kimambo.

Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Huduma za Ukunga na Uuguzi, Bi Redemptha Matindi, amemshukuru Dkt. Kimambo kwa kutenga muda kuzungumza na wafanyakazi hao, na kusisitiza kuwa kurugenzi yake itaendelea kuzingatia maelekezo na ushauri uliotolewa ili kuhakikisha MNH inabaki kuwa kimbilio la kila mmoja.

Dkt. Kimambo amewahimiza wahudumu hao kushirikiana kwa karibu na idara nyingine, akisisitiza kuwa mafanikio ya hospitali yanategemea mshikamano na moyo wa kuwahudumia wananchi kwa pamoja.

spot_img

Latest articles

Waziri Aweso: Tuna uhakika wa maji ya kutosha Dar na Pwani

Na Mwandishi Wetu WAZIRI wa Maji, Jumaa Aweso amewatoa hofu wakazi wa mikoa ya...

PURA yajivunia mafanikio katika Ajenda ya Nishati Safi na ushiriki wa Watanzania Sekta ya Mafuta na Gesi

Na Tatu Mohamed MAMLAKA ya Kudhibiti Mkondo wa Juu wa Petroli (PURA) imesema inajivunia...

Machungu, damu yamwagwa tena

Maadhimisho ya Saba Saba nchini Kenya ni tukio muhimu katika kukumbuka mapambano ya kudai...

eGA yatumia Sabasaba kuelimisha umma kuhusu Mfumo wa e-Mrejesho, yajivunia Tuzo ya Kimataifa

Na Tatu Mohamed MAMLAKA ya Serikali Mtandao (eGA) imeendelea kuonesha namna ambavyo Serikali inavyotekeleza mageuzi...

More like this

Waziri Aweso: Tuna uhakika wa maji ya kutosha Dar na Pwani

Na Mwandishi Wetu WAZIRI wa Maji, Jumaa Aweso amewatoa hofu wakazi wa mikoa ya...

PURA yajivunia mafanikio katika Ajenda ya Nishati Safi na ushiriki wa Watanzania Sekta ya Mafuta na Gesi

Na Tatu Mohamed MAMLAKA ya Kudhibiti Mkondo wa Juu wa Petroli (PURA) imesema inajivunia...

Machungu, damu yamwagwa tena

Maadhimisho ya Saba Saba nchini Kenya ni tukio muhimu katika kukumbuka mapambano ya kudai...