Na Mwandishi Wetu
Yanga imefanikiwa kutetea ubingwa wake wa Ligi Kuu Tanzania Bara kwa kuichapa Simba mabao 2-0, kwenye Uwanja wa Benjamini Mkapa, Dar es Salaam. Ubingwa huo unakuwa wa mara ya nne mfululizo na mara ya 31 tangu kuanzishwa kwa ligi hiyo.
Katika mechi hiyo ya kibabe iliyokuwa inaamua bingwa ni nani baada ya vuta ni kuvute za kuahirishwa kwa mchezo huo, mabao ya Yanga yalifungwa na Pacome Zouzoua dakika ya 66 kwa mkwaju wa penalti na Clement Mzize dakika ya 86.

